Mabingwa wa soka Tanzania, Simba wameendelea kujifua vilivyo licha ya hali ya hewa ya ukungu.
Hali ya hewa ya ukungu imetanda katika enero la milima ya Kartepe nchini Uturuki, lakini chini ya Kocha Patrick Aussems raia wa Ubelgiji, Simba imeendelea kujifua.
Kikosi hicho kimeweka kambi nchini Uturuki na kimekuwa kikiendelea na mazoezi yake kama kawaida.
Simba inajiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Bara lakini mashindano mengine mbalimbali yakiwemo ya kimataifa.








0 COMMENTS:
Post a Comment