July 23, 2018



Mesut Ozil amejiondoa kuichezea timu ya taifa ya Ujerumani akisema amestaafu kwa sababu ya UBAGUZI WA RANGI na DHARAU kutoka kwa Chama cha Soka Ujerumani (DFB) na mashabiki.

Ozil mwenye asili ya Uturuki amekuwa akituhumiwa kuonyesha kiwango duni wakati wa Kombe la Dunia nchini Urusi ambako Ujerumani ilivuliwa ubingwa.

Hadi anatangaza kustaafu soka la kimataifa, Ozil ameichezea Ujerumani mechi 92, amefunga mabao 23.
Aliisaidia kubeba Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil. Mwaka 2012 walifika nusu fainali ya Euro na 2016 wakabeba ubingwa.

Alianza kuichezea timu ya taifa ya Ujerumani mwaka 2009  na 2010 alikuwa katika kikosi kilichoshiriki Kombe la Dunia kama 2018.

#salehjembeupdates

1 COMMENTS:

  1. Wengi hawalisemei hili; may be kwa sababu hawawafahamu Wajerumani vizuri..
    Lakini kiasili Wajerumani ni wakatili, wabaguzi na watu wenye dharau za hali ya juu!!

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic