July 20, 2018


Na George Mganga

Uongozi wa klabu ya Simba kupitia Makamu Rais wake, Salim Abdallah 'Try Again' umefunguka juu ya kushindwa kukaa na makocha kwa muda mrefu.

Abdallah amesema klabu inapoajiri kocha yeyote muda wake unapomalizika huondoka kama ilivyokuwa kwa aliyekuwa kocha Mfaransa Pierre Lechantre.

Kauli hiyo imekuja kufuatia Simba imekuwa ikibadili makocha ambao wengi kwa takribani miaka saba ambao wengi wao wameshindwa kumaliza msimu mmoja.

Abdallah ameeleza Simba waliamua kuachana na Lechantre kwasababu aliomba nafasi ya kazi Cameroon, hivyo kwa busara kama uongozi wakaona ni vema busara ikatumika baada ya mkataba wake kumalizika.

Ikumbukwe Lechantre, alikuja nchini kuchukua mikoba ya Mcameroon, Joseph Omog aliyefukuzwa kazi kutokana na uongozi wa Simba kushindwa kuridhishwa na utendaji wake katika kikosi cha wekundu wa Msimbazi.

Baada ya kuachana na Mfaransa huyo, jana Simba imeingia mkataba na Kocha mpya, Mbelgiji, Patrick Aussems, aliyesaini mkataba wa mwaka mmoja.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic