FEI TOTO AMPONZA AJIBU YANGA
Kocha Mkuu wa Yanga, Mkongomani, Mwinyi Zahera amefurahishwa na umakini wa upigaji pasi safi zilizonyooka wa kiungo wake, Feisal Salim ‘Fei Toto’ huku akimtaka kiungo mshambuliaji, Ibrahim Ajibu kumuiga nyota huyo.
Kauli hiyo aliitoa baada ya kumalizika kwa mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda ambayo ilimalizika kwa Yanga kufungwa bao 1-0, huku Ajibu akicheza namba 10 ambayo Zahera amekuwa akimpanga Fei Toto.
Ajibu ambaye hivi karibuni alikuwa hana nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha Zahera alionyesha kiwango kizuri sana kwenye mechi hiyo.
Akizungumza na Championi Jumatano, Zahera alisema mshambuliaji huyo ana tatizo kubwa la kupoteza pasi nyingi katika mechi ambalo hataki kuona likiendelea kwenye michezo ijayo ya ligi.
“Siku zote upotezaji wa pasi unatokana na mchezaji kutokuwa makini, ili mchezaji apige pasi safi ni lazima awe makini.
ajitathmini sasa hasa goal yake
ReplyDelete