September 6, 2018


Patrick Aussems ameweka wazi kwamba mbinu pekee ambayo itaipa ubingwa Simba kwa msimu wa pili mfululizo ni kutopoteza pointi yoyote kwenye mchezo wao ambao watacheza nyumbani na watatakiwa kukusanya pointi 57 ambazo watazig­ombania.

Kocha huyo raia wa Ubelgiji ambaye tayari ameshaiongo­za Simba kwenye michezo mi­wili ya ligi kuu hadi sasa bado ana kibarua cha michezo 17 ijayo ambayo watakuwa wanaichezea katika Uwanja wa Taifa jijini Dar ambao wamekuwa wakiutumia kama uwanja wao wanapokuwa na michezo ya nyumbani.

Kocha huyo ambaye ame­saini mkataba wa mwaka mmoja na Simba ameliam­bia Championi Jumatano, kuwa ameamua kufanya hivyo kutokana na kufa­hamu wazi juu ya ugumu ambao watakutana nao kwenye michezo yao ya ugenini ambayo itakuwa kazi ngumu kwao kutokana na kutokuwa na mazingira rafiki ya kuchezea tofauti na vile ambavyo watacheza kwenye Uwanja wa Taifa.

“Siyo mbaya hadi sasa tumecheza michezo miwili hapa nyumbani na tume­fanikiwa kushinda yote, hiyo imetokana na jinsi ambavyo tulivyojiandaa vizuri lakini bado tuna kazi kubwa ya kuifanya kwenye michezo yetu inayokuja.

“Unajua kwamba tumean­zia hapa nyumbani na baada ya muda mfupi tutaanza kuto­ka kwenda ugenini hivyo hili tusiende kupata shida sana huko nimepanga ni lazima kwamba tushinde michezo yetu iliyobakia ya hapa nyumbani ili tu­punguze presha pale ambapo tutaanza kwenda huko mkoani kwa sababu naelewa mazingira ya kucheza ugenini kwamba kuna mazingira yasiyo rafiki sana kwa wachezaji kupata matokeo,” alisema Kocha huyo.

Simba itacheza michezo 38 am­bapo michezo 19 watacheza kwenye uwanja wa nyumbani na michezo mingine 19 wataicheza katika viwanja mbalimbali wakiwa ugenini vikiwemo Mkwakwani, Tanga na Kirumba, Mwanza.

3 COMMENTS:

  1. Kila timu ina malengo hayohayo

    ReplyDelete
  2. tunahitaji ushindi hata ugenini tuna kikosi kipana .hakuna haja ya kuitaji ushindi wa nyumbani pekee, nikukaza tu kamaba tu kamba

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic