September 19, 2018


Kwa mara ya kwanza juzi Jumatatu kiungo wa Simba, Mnyarwanda, Haruna Niyonzima na Mganda, Juuko Murshid, wameanza mazoezi rasmi chini ya kocha wake mkuu, Mbelgiji Patrick Aussems kwa msimu huu.

Wachezaji hao wote wa Simba walikuwa hawapo ndani ya kikosi hicho kutokana na kuwa na matatizo tofauti na mara baada ya kumaliza majukumu yao ya timu za taifa walirejea nchini huku timu ikiwa Mtwara kucheza na Ndanda.

Niyonzima na Juuko walikaa na uongozi wa klabu hiyo na kuweza kumaliza tofauti zao kisha waliomba radhi na kurudishwa kundini kama awali.

Wachezaji hao walifika mazoezini hapo na kukabidhiwa jezi na kuanza mazoezi ambayo yalikuwa yanaendelea kuelekea mchezo wao dhidi ya Mbao FC ambao utapigwa kesho jijini Mwanza.

Mbelgiji alisema kuwa wachezaji hao wameanza mazoezi ila ataendelea kuwaangalia kwanza na suala la wao kuweza kucheza mchezo ujao bado wanahitaji muda.

“Wachezaji ndiyo kama ambavyo mmewaona hapa wanaendelea na mazoezi wamekuja na wataendelea kufanya mazoezi na suala la kusema watacheza mechi ya kesho, hilo wanahitaji kupewa muda kujifua zaidi,” alisema kocha huyo kwa ufupi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic