September 19, 2018


Manchester City bado hawajaanza mazungumzo ya mkataba na wing'a mwenye miaka 23 Raheem Sterling, lakini sasa wanataka kufanya mazungumzo kuhusu kuongeza mkataba huo ambao utakamilika mwaka 2020. (Sun)

Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair ametajwa k amamtu anayeweza kuwa mwenyekiti wa siku za usoni wa shirika linalosimamia Ligi ya Premia. Hilo lilifanyika wakati wa mazungumzo ya hivi karibuni ya klabu za England. (Daily Mail)

Brighton wanataka kumteua mkurugenzi wa kiufudi wa FA Dan Ashworth katika nafasi sawa na hiyo kwenye klabu yao.

Mlinzi wa Leicester raia wa England mwenye miaka 25 Harry Maguire amekana ripoti kuwa wachezaji hawakufurahishwa baada ya wao kusafiri kwa magari badala ya ndege kwa mechi huko Bournemputh. (Leicester Mercury)

Afisa mmoja wa West Brom aliondoka klabu hiyo baada ya uamuzi wa kukosa kununuliwa Virgine van Dijk kutoka Celtic licha ya kumpendekeza. (Scottish Sun)


Ajenti wa Mesut Ozil amewakashifu Manuel Neuer, Thomas Muller na Toni Kroos kufuatia matamshi waliyotoa baada ya uamuzi wa kiungo huyo wa kati wa Arsenal wa kuacha kuichezea Ujerumani mechi za kimataifa. (Guardian)

Meneja wa England Gareth Southgate alienda kutazama mechi ya nyumbani kati ya Derby na Blackburn Rovers badala ya mechi la ligi ya mabigwa kati ya Liverpool na Paris St-Germain siku ya Jumanne. (Times)

Meneja wa zamani wa Sunderland Gus Poyet anasema angetaka tena kusimania klabu ya England. (South China Morning Post)


Mwekezaji mmoja huko Uruguay ambaye ana hisa huko Sunderland anasema ana mpango kabambe wa miaka mitatu kusaidia kurejesha klabu hiyo katika Ligi ya Premio. (Northern Echo)

Kutoka BBC

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic