November 5, 2018


Mshambuliaji wa timu ya Simba Meddie Kagere raia wa Rwanda amefunguka na kusema kuwa anafanya kazi kwa kujituma na ataendelea kupambana kuhakikisha anaisaidai timu yake kufanya vizuri na kutaja siri ya kufanikiwa kwake.

Kagere alifanikiwa kufunga mabao 2 ambayo yaliipa pointi tatu Simba mbele ya JKT Tanzania katika mchezo uliochezwa uwanja wa Mkwakwani Tanga na kufanya waweze kushinda mchezo wao wa 8 wakiwa na sare mbili na wamepoteza mchezo mmoja kati ya 11 waliyocheza.

 Kagere amesema kuwa anaona fahari kuisaidia timu yake kushinda ataendelea kufanya hivyo kila anapopata nafasi kwa kuwa hicho ndicho kimemleta Simba kucheza na kupata matokeo.

"Uwezo wa kusubiri na kuendelea kufanya jambo ingawa ni gumu bila kulalamika pamoja na nidhamu, kujituma nikiwa ndani na nje ya uwanja kunafanya niweze kufanya vizuri kila ninapopata nafasi hili ni jambo la kushukuru.

"Ushirikiano uliopo ndani ya timu, pia naamini mwenyewe kile ambacho nakifanya bila kuwa na hofu ndani ya uwanja, nawapenda sana mashabiki wangu nawafikiria sana muda mwingi hivyo sina cha kuwambia zaidi ya kuwashkuru kwa kunikubali pamoja na kunipokea vizuri," alisema.

Kagere anafikisha mabao 7 kwa wafungaji akiwa amefungamana na Emmanuel Okwi wote wakiwa ni washambuliaji wa kimataifa huku namba moja akiwa ni mzawa Eliud Ambokile ambaye ana mabao 8.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic