January 19, 2019





Nahodha wa timu ya Stand United, Jacob Massawe ameonyesha thamani yake mbele ya wapinzani wao wa muda mrefu Yanga kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa leo Uwanja wa Kambarage.

Masawe alifunga bao pekee na la ushindi dakika ya 88 kwa kichwa akitumia makosa ya mabeki wa Yanga ambao walimpa nafasi ya kupiga kichwa kilichompoteza Klaus Kindoki.

Licha ya Yanga kuongoza kwa kumiliki mpira walishindwa kutibua mipango ya Stand United,' Chama la wana' walifanikiwa kulinda ushindi wao.

Stand United wanafanikiwa kuvunja rekodi ya Yanga baada ya kucheza michezo 19 bila kupoteza leo wanapoteza mchezo wa kwanza wakiwa ugenini kwa bao la usiku.

12 COMMENTS:

  1. Raha ya kuchezea nje ya Dar!

    ReplyDelete
  2. Sasa wimbo wa viporo...viporo utasikika!kama kwamba mwaka juzi na Jana wao walikuwa hawana viporo!

    ReplyDelete
  3. Mwabeja sana shinyanga! Bado Mwanza na Musoma...Kanda maalumu

    ReplyDelete
  4. Kwani kumetokea nini?
    Nasikia vigelegele mwali kabikiriwa nini?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ha ha haaaaaaaaaa, imenifurahisha saaaaana! "Mwali Kabikiliwa" huyo atakuwa ni "Bikra Kidawa".

      Delete
  5. Yeah mwali wamefanywa mbaya na vibonde vilivyo nafasi ya 16...afadhali mikia fc walitendwa na walio nafasi ya 5!

    ReplyDelete
  6. Huyu jamaa yanga isipofanya vizuri hatumi habari kwawakati,kulikon?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Saleh jembe ndivyo walivyo..wakifunga Yanga wanaweka matokeo fasta hata iwe mechi ya SAA mbili usiku..Ikicheza simba usiku ikashinda unakuta had SAA tano asubuhi Sikh inayofuata hawajaweka matokeo..jifunzeni kwa bin zuberi.sio sawa kuegemea upande mmoja

      Delete
  7. Has saleh jembe kulikoni...kichwa cha habari hapo kinaonyesha mlikuwa mnafuatilia mechi!mbona matokeo hamweki..

    ReplyDelete
  8. Angekuwa Makambo kafunga hapo mngekuwa mmeweka..zaidi ya nusu SAA tangu mechi imeisha...Bin zuberi keshaaandika..".Wametobolewa"

    ReplyDelete
    Replies
    1. Sio nusu saa tu, pale pale goli linapofungwa utasikia "kwasasa ni dakika ya 75 Makambo anaitanguliza Yanga kwa Goli la kibabe!". Yaani hapo kila dakika inapobadilika utapata taarifa hadi dakika ya 90. Utasimuliwa hadi faulo zote na kona zote na dakika zake!

      Delete
  9. Blog hii mimi mwisho leo.Shafi Dauda alianza hivi hivi blog imemfia mkononi. Hakuna wasomaji.
    Hii nayo imeanza kuleta chuki nä habari za upande mmoja dawa ni kuisusa.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic