January 19, 2019


Kikosi cha Yanga kimekubali kupoteza mchezo wake wa kwanza kwenye Ligi Kuu Bara katika mchezo uliopigwa CCM Kambarage Shinyanga dhidi ya Mwadu FC kwa bao 1-0.

Bao pekee la mchezo huo limewekwa kimiani na Jacob Masawe mnamo dakika ya 88 ya mchezo kunako kipindi cha pili.

Ushindi wa Stand unaifanya Yanga iendelee kusalia kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na alama zake 53 ikiwa imeshacheza michezo 20.

Katika msimu huu tangu kuanza, Yanga ilikuwa haijapoteza mchezo wake hata mmoja zaidi ya kwenda suluhu na Ndanda FC kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Matokeo hayo pia yanaifanya Stand kufikisha alama 25 ikicheza jumla ya mechi 23 mpaka sasa.

11 COMMENTS:

  1. Inginia somaaaa!!!!!
    hongera sana jacobo massawe kwa kupeleka kilio jangwani, hongera chama la wana.

    ReplyDelete
  2. Replies
    1. Afadhali hao wamefika makundi Kinshasa.. Miaka yote Yanga walikuwa wanaishia wapi?

      Delete
    2. Kikotoo kipya kimewabeba, kingetumika cha zamani mngeishia njiani kitambo...
      ila mlijitapa sana, mpira sio taarabu

      Delete
  3. Afadhali kufungwa 5 na Vita kuliko kufungwa 1 na timu ya 16 kwenye ligi ya Bongo.

    ReplyDelete
  4. Kufeli chekechea na kufeli kidato cha 4 ipi aibu?
    Matundu 5 mengi...
    Bado yale ya Mashujaa, hivi wapo nafasi ya ngapi TPL?

    ReplyDelete
  5. Kwa hiyo unajua nani yupo chekechea na nani yupo form 4.
    Kwa hiyo hawalingani.
    Nyie bado mnanuka maziwa.Malindi wapo wa ngapi vile?
    Nasikia mnataka Kakolanya arudi.Bikra ndio imevunjwa na Stendi sasa kila mmoja atajilia tu.Subiri uone.

    ReplyDelete
  6. Mwandishi, check paragraph ya kwanza, sio Mwadui ni Stand ndio waliotoa bikra ya mtu. Sasa hapo Stand wameshang'oa Koki, subiri uone maji yatakavyomwagika. Mlipohesabu mechi nne za ubingwa, hii ya stand hamkuihesabu. Kwahiyo zimebaki nne zilezile.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic