LIGI Kuu Tanzania Bara leo inaendelea ikiwa ni mzunguko wa 21 ambapo jumla ya timu sita zitashuka Uwanjani kutafuta pointi tatu muhimu.
Michezo yote leo itachezwa saa 10:00 jioni huku kila timu ikiwa imejipanga sawasawa kwa ajili ya ushindani huo na kuwaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi kuona namna ushindani utakavyokuwa.
KMC wataikaribisha Ruvu Shooting Uwanja wa Uhuru, saa 10:00 jioni, Lipuli wataikaribisha JKT Tanzania, Uwanja wa Samora Iringa saa 10:00 jioni na Mwadui FC wataikaribisha Singida United, Uwanja wa Mwadui Complex Shinyanga saa 10:00 jioni.
0 COMMENTS:
Post a Comment