April 15, 2019


Simba Simba Simba,kama ilivyo desturi yangu nnapoandika kitu SIRIAZI hutumia Tanakudi tatu kwa msisitizo!!

Yes. Wanasimba wote kuanzia viongozi,wanachama,wachezaji,benchi la ufundi na washabiki wetu wapendwa nyie ni washindi!!

Mlikuwa na lengo la kufikia Group stage halaf mkalivuka!

Mmeweka heshma ya kumaliza ligi hii ngumu ya mabingwa watupu bila kufungwa hata mechi moja nyumbani,mmejitangaza kote Afrika na mlibaki timu nane tu ktk kundi la timu zaidi ya laki moja zilizotapakaa kote barani Afrika!!

Na hakika yenu nyie ndio mtakuwa mabingwa tena wa nchi hii msimu huu,so mtarudi tena next season na nnamiini mtarudi kwa nguvu kubwa!!

Guys waacheni wanaowatania leo ila msijadiliane nao coz kujadiliana nao kuhusu ligi hii kubwa ni sawa na kumwelekeza Mtoto mchanga raha ya tendo la ndoa!!

Kalijulia wapi na yeye yake nepi?

Na Haji S Manara

15 COMMENTS:

  1. Zahera kihiyo....soma hiyooo

    ReplyDelete
  2. AACHE KUITAJA YANGA ABAKI AKISHUGHULIKA NA HABARI ZA SIMBA YAKE KAMA ATAWEZA!!!
    BILA KUITAJA YANGA HUNA KIKI BRO !!
    MMEFUNGWA NA MAZEMBE SASA YANGA YAWAHUSU NINI HAPO !!

    ReplyDelete
  3. Wapi kaitaja Yanga!Jiwe imetupwa gizani ukitoa mguno shauri yako.
    Zahera ndio mpe huo ushauri kwani yeye kila akifungua mdomo Simba utafikiri ni kocha wa Simba.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Zahera anahojiwa na media kuhusu Simba anajibu kuhusu Simba ulitaka aulizwe Simba ajibu Yanga mbona uelewa wako mdogo sana

      Delete
  4. Sareh acha kuandika ujinga wa MANARA kama umekosa habari tafuta kazi nyingine za kufanya, hata udobi ni kazi bro. Kazi ya habari imekushinda una copy na ku paste ujinga.

    ReplyDelete
  5. Mbona akihojiwa Aussems hataji timu nyingine?Makocha wote wenye uweledi hasa wa nje,hukuti akizungumzia timu zingine.
    Labda waandishi hawana cha kuuliza kuhusu Yanga?Waulize kuhusu michango?
    Kocha anatakiwa azungumzie timu yake full stop.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mhh aliulizwa onaonaje mchezo wa Mazembe na Simba???? Akajibu anavyoona yeye ulitaka ajibu nini???? Akikataa kujibu maneno yanakua mengi wabongo bana shida tupu

      Delete
    2. Aussems kahojiwa lini kuhusu Yanga????? Ongea facts sio ushabiki

      Delete
    3. Wakatazeni Waandishi, wasimuulize Zahera habari za Simba sio kutoa mapovu tu,Yeye siyo kichaa aulizwa habari za yanga halafu aseme simba, Msipotoshe watu

      Delete
  6. Hata akihojiwa kuhusu Simba angejibu mimi sio kocha wa Simba!
    Amekuwa mropokaji kwenye kila kitu.
    Silence is gold .

    ReplyDelete
  7. Simba ndio habari.Migongo wazi waandishi wamechoka. Kila mara migogoro,timu haina viongozi. Kocha dikteta. Leo anamfukuza Ajibu kesho anamuita. Kwanini Ajibu asiringe?Wataripoti michango,wachezaji kukimbia njaa!

    ReplyDelete
  8. Kwa Mtu mwenye busara lugha ya matusi ni udhaifu...Manara,Manara,Manara,Jiheshimu kwanza ndipo Utafute heshima kwa wengine,usiwe na mihemko mpira ndivyo ulivyo.LUGHA CHAFU YA NINI HAPA????.Tafakari ulikosea wapi urekebishe,Kutukana siyo jadi ya Watanzania,Utani upo na utaendelea kuwepo hata utoe MAPOVU Kiasi gani,..TP MAZEMBE siyo Tanzania.

    ReplyDelete
  9. Wapi katukana,?Roho mbaya mmezoea hata linalowafaidi mnapinga.
    Kuchagua viongozi mnashindwa inabidi msimamiwe kama mna nepi!
    Lakini kwa husda na majungu mna ubingwa wa dunia.
    Toeni boriti kwenye jicho lenu kabla hamjazungumzia ubanzi kwenye jicho la jirani.

    ReplyDelete
  10. Migongo wazi. Michango ya TASAF inaendeleaje?

    ReplyDelete
  11. Tatizo hapa co yanga bali why hatushindi ugenini? Tusijivunie kutofungwa dar tujiulize kp kgumu ugenini kila wakituona wanatuogesha?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic