WANNE WASHUSHWA YANGA KUIPA CHANGAMOTO SIMBA, JEMBE MOJA KUTOKA NIGERIA
Imeelezwa kuwa Kocha mkuu wa klabu ya Yanga SC, Mwinyi Zahera ameshusha majembe yake manne kutoka nje ambayo ni Mshambuliaji wa Nigeria Victor Patrick Akpan kutoka JKU ya Zanzibar na Beki wa kati Mohamed Ali Camara 'Pique' kutoka Horoya ya Guinea aliyekuwa anacheza Young Boys kwa mkopo.
Wengine ni shambuliaji kutoka Nigeria, Shehu Magaji Bulama na Kiungo Allex komenan kutoka Ivory Coast.
Wachezaji hao wote wanne wapo nchini wanafanya mazoezi na klabu ya Yanga kabla ya kuamua kuwapa mikataba.
Taarifa imeeleza kuwa Kocha wa klabu ya Yanga amepanga kusajili wachezaji 6 wapya wa kimataifa.
Hizo picha za man u vs wolves za nn??
ReplyDelete