July 5, 2019


KIKOSI cha Simba ambacho kinaendelea kujiimarisha kwa ajili ya msimu mpya wa mwaka 2019-20 mpaka sasa tayari wamemalizana na wachezaji wa kigeni tisa kutoka mataifa tofauti.

Wachezaji hao watatu ni kutoka  Brazili huku wengine wakiwa wanatoka ndani ya bara la Afrika kama ifuatavvyo:-

Meddie Kagere mshambuliaji wa Simba ameongeza mkataba wa miaka miwili yeye ni raia wa Rwanda na anakipiga pia timu ya Taifa ya Rwanda.
Clatous Chama, raia wa Zambia anayekipiga pia timu ya Taifa ya Chipolopolo  ameongeza kandarasi ya miaka miwili yeye ni kiungo.

Sharaf Eldin Shoboub Ali Abdalrahman, kiungo raia wa Sudan amesaini kandarasi ya mwaka mmoja ametokea timu ya Al Hilal ya Sudan.

Wilker Henrique da Silva raia wa Brazil amesaini kandarasi ya miaka miwili ametokea Bragantino.


Gerson Fraga Veira ametokea ATK FC ya India yeye ni raia wa Brazil amesaini kandarasi ya miaka miwili.


Beki Tairone Santos da Silva raia wa Brazil amesaini kandarasi ya miaka miwili ametokea timu ya Atletico Cearense FC ya Brazil.

Sergio Wawa raia wa IvoryCoast yeye ni beki kisiki ndani ya Simba ameongeza kandarasi ya mwaka mmoja.


Deo Kanda yeye ni mshambuliaji raia wa Congo amesaini kandarasi ya mwaka mmoja

Francis Kahata yeye ni raia wa Kenya amejiunga na Simba kwa kandarasi ya miaka mwili akitokea timu ya Gormahia na anakipiga pia kwenye timu ya Taifa ya Kenya kwa nafasi ya kiungo.

4 COMMENTS:

  1. Gadieli Michael ni mbovu sana kwenye kukaba magoli mengi ya Timu ya Taifa na hata mechi za ligi kuu yalikuwa yanapitia upande wake fuatilia mechi za Taifa Stars na za Yanga utakubaliana namimi....Kama mimi ndio nasajili Simba natafuta namba 3 ni mara mia nimchukue Godfrey Walusimbi kuliko Gadieli Michael....yeye (Gadieli) ni mzuri tu kwenye kushambulia....kitu ambacho Mohamed Husein Tshabalala anacho na zaidi

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic