July 31, 2019


PATRICK Aussems, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa uwezo wa wachezaji wake umeimarika hivyo ana imani kubwa watakuwa na kitu cha kipekee msimu ujao.

Simba jana ilifunga hesabu nchini Afrika Kusini kwa kutoka sare ya kufungana bao 1-1 na Orlando Pirates mchezo wa kirafiki uliochezwa Afrika Kusini.

Aussemss amesema:-"Tumemaliza kambi na Orlando Pirates ambao wapo tayari kuliko sisi wao wametumia muda mwingi kujiaandaa kwa ajili ya msimu ujao tofauti na sisi.

"Napenda kuwapongeza wachezaji wangu tulikuwa na wakati mzuri sana Rustenburg, kila mmoja kafanya kazi nzuri tunaweza kusema hii kambi imekuwa nzuri sana na nimeridhishwa kwa hatua ambayo tumefika," amesema.

6 COMMENTS:

  1. Sasa tunautaka ubingwa Kwa mara ya tatu mfululizo na kama si kuuchukuwa ubingwa Kwa mechi za klabu bingwa Afrika, tufike mbali Zaidi kuliko tulipofika msimu uliyopita kwasababu Hali ya Simba ni marudufu bora kuliko misimu yote iliopita

    ReplyDelete
  2. kambi iliyogawanyika wachezaji yumkni haikufikia malengo

    ReplyDelete
  3. Ipi ilikuwa haijagawanyika?Umejuaje kwamba haijafikia malengo?Wewe ni Aussems?

    ReplyDelete
  4. Tunataka kuona simba ikiwa kiwango cha juu sana

    ReplyDelete
  5. Walchezaji kadhaa muhimu wa Yanga wamegomea kambi huko ndiko kugawanyika.

    ReplyDelete
  6. Yaliyobakia mi maneno lakini myama hata Huko Afrika Kusini wametaja waziwazi kuwa kiwango cha Mnyama kinatisha

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic