MICHUANO ya Afcon
kwetu sisi ilikuwa ni changamoto mpya kwani tumeona namna gani timu yetu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ ikihaha kupata matokeo chanya kutokana na
kutokuwa na uzoefu mkubwa.
Kwetu sisi
kwa hatua ambayo tumefikia si mbaya ila kuna mengi ya kujifunza ambayo ni
lazima tuyafanyie kazi kwa ajili ya maboresho wakati mwingine tukipata nafasi
ya kushiriki michuano hii mikubwa.
Tumeshuhudia
kwa macho yetu mchezo wa kwanza dhidi ya
Senegal ambao tulipoteza kwa kufungwa
mabao 2-0 namna ambavyo mashabki waliumia na kulalalamika kutokana na mfumo wa
mwalimu.
Mchezo wa pili
tuliona kulikuwa na mabadiliko makubwa hasa kwa timu kucheza na kupata matokeo
jambo ambalo kwa kiasi fulani lilileta matumaini kwa timu yetu kuonyesha uwezo
wake
Licha ya
kupoteza mchezo wetu mbele ya Kenya bado kulikuwa na kitu ambacho kilifanywa na
wachezaji wetu ambao walipambana kipindi cha kwanza lakini kipindi cha pili
mbinu ziliwakataa wakazidiwa ujanja na kupoteza kwa kufungwa mabao 3-2.
Mchezo wa mwisho ukawa funga kazi baada ya kupoteza kwa mabao 3-0 mbele ya Algeria hakuna namna nyingine zaidi ya kuvuna kile tulichopanda.
Tuna kitu
ambacho tunapaswa tujifunze kwa wenzetu ambao wamefanikiwa kutinga hatua ya 16
bora kwenye michuano hii ya Afcon ama wale ambao walipata fursa ya kulinda
matokeo yao ambayo walikuwa wakiyapata kwenye michuano hii mikubwa Afrika.
Wenzetu
asilimia kubwa ukitazama kikosi chao robo tatu ya wanaounda kikosi cha kwanza wanacheza
nje ya nchi hali inayowafanya wawe bora kutushinda sisi ambao asilimia kubwa
wachezaji wetu wanacheza ligi ya ndani.
Hali hiyo
ipo kwetu pia kwani wale wachezaji ambao
wanacheza ligi ya nje wanafanya vizuri
tofauti na wale ambao wanacheza ligi ya ndani hapa kuna kitu Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF) wanapaswa wafanye.
Mtazame
mchezaji kama Mbwana Samata, Simon Msuva,
Farid Mussa,Thomas Ulimwengu namna wanavyoonyesha kandanda ambalo si la kawaida
hasa kwa kucheza kwa ufanisi mkubwa uwanjani.
TFF
wanapaswa waangalie namna ya kukuza ligi yetu iwe bora kuliko vile ambavyo ipo
sasa ili kutoa fursa ya kutengeneza wachezaji bora na imara ambao itakuwa
rahisi kwao kujiuza nje ya nchi.
Kwa wale wa
Tanzania ambao wanacheza ligi ya ndani
wapo baadhi ambao nao wamekuwa ni bora na ukiwafuatilia kwa ukaribu
utagundua kwamba wamekuwa na misingi mizuri tangu awali.
Kutoka chini
wamejengwa vizuri hasa kwa kupitia kwenye vituo vya kuwakuza pamoja na kupata
walimu wazuri ambao wanawapa changamoto mpya kila siku jambo ambalo linawafanya
nao wawe kwenye chati.
Jambo lingine
la ajabu ambalo linapatikana kwenye ligi yetu ni namna wageni ambao wanakuja
kucheza ligi yetu wanavyokuwa bora kushinda wazawa hasa kwenye timu za Taifa.
Hapa pia
wachezaji wetu wanapaswa kujifunza namna bora ya kulinda viwango vyao pamoja na
kujituma bila kujali aina ya timu ambayo wanachezea ili kulinda uwezo.
Kujitambua
kwa wale ambao wanacheza ligi zetu kunawapa nafsi ya wao kufanya vizuri hata
wanapokuwa nje ya timu zetu za Bongo ambazo zinawapa nafasi ya kucheza.
Cheki
Emmanueli Okwi, Juuko Murshid, Thaban Kamusuko, Tafadzwa Kutinyu
hawa wanafanya vizuri wakiwa kwenye timu zao za Taifa na wametoka ligi yetu.
TFF iangalie
namna ya kubadili watu wa ndani wawe na uimara hata wanapotoka nje misingi bora ya kusimamia ligi yetu inatosha
kuwafanya vijana wetu kuwa imara wakati wote kitaifa na kimataifa.
Ligi iwe
bora itasaidia kuwapata wachezaji makini ambao watatupa matokeo chanya kwenye
michuano mingine inayofuata na sio kuishia kuwa wasindikizaji.
Tumeona
wenzetu wa Cameroon, Uganda wamekuwa wakiwaita wachezaji wakubwa kutoa hamasa,
sasa kwetu imekuwa tofauti wamekwenda wanasiasa jambo ambalo linaleta mkanganyiko.
Afcon
isituache wapekwe bali itupe somo wakati mwingine tunapaswa nasi tuwape nafasi
malegendari wetu ambao wamecheza Afcon, watu kama kina Peter Tino, Edibly
Lunyamila, hawa wapewe nafasi ya kuzungumza na wachezaji.
Tusichanganye
siasa na mpira ni vitu viwili tofauti itakuwa ngumu kwetu kufikia mafanikio
kama tutakubali mpira utawaliwe na siasa.
Wanasiasa
wana nafasi zao na sehemu zao za kufanya kazi lakini si kwenye mpira kutoa
hamasa ni jambo la kiupekee haina maana kwamba hawapaswi kushangilia timu yao TFF
itofautishe haya mambo mawili tofauti kabisa kushangilia na kutoa hamasa.
Timu ya Taifa inatolewa AFCON....Turudi sasa kwenye "vumbi letu na usajili wa magazeti na mihemko ya ushabiki wa timu za Kariakoo zinazodumaza soka letu"
ReplyDeleteSaleh Jembe .Atom Haifanyi Kazi Ukibofya Inaleta Habari Za Zamani (50 Day Ago)
ReplyDelete