August 25, 2019



KIUNGO bora wa Simba kwa msimu wa mwaka 2018/19, James Kotei ambaye kwa sasa anakipa Kaizer Chief amesema kuwa Simba ina nafasi kubwa ya kushinda mchezo wake wa leo dhidi ya UD do Songo ya Msumbiji endapo wachezaji watakuwa na nidhamu.

Akizungumza na Saleh Jembe, Kotei  amesema kuwa kwa namna Simba ilivyo na moto ikiwa uwanja wa Taifa ni nafasi ndogo kwa wapinzani wao kupenya kirahisi.

“Nimekuwa ndani ya Simba kwa muda mrefu, nimeona namna mashabiki ambavyo wanaipenda kutoka moyoni timu yao na ule wingi wao namna unavyowabeba wachezaji basi ushindi wa kwanza umejificha kwa mashabiki.

“Hakuna kitakachowazuia Simba kushindwa kupata matokeo wakiwa Taifa, usajili wao ni mzuri na wana wachezaji makini kama Shiboub (Sharaf), Kahata (Francis) naamini wachezaji wakijiamini kiasi na kuwaheshimu wapinzani basi ushindi ni halali yao,” amesema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic