August 25, 2019


MASHINDANO ya kumtafuta bingwa mpya wa michuano ya Sprite B Ball Kings kwenye mchezo wa kikapu yamezidi kupamba moto ambapo leo kwenye viwanja vya JMK Parks mchakato wa kutafuta timu 16 bora ulianza.

Bingwa mtetezi Mchenga Boys tayari ameshafuzu hatua ya 16 bora na kufanya timu 15 kutafutwa kutinga hatua ya 16 bora kwa ajili ya kuendelea safari ya kumtafuta bingwa mpya.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Sprite B.Ball Kings, Goza Chuma amesema kuwa mashindano ya msimu huu yamekuwa na msisimko wa kipekee kutokana na timu nyingi kujitokeza.


“Msimu huu timu nyingi zimejitokeza na zimeonyesha ushindani wa kweli tunatarajia kesho kuchezesha droo ya timu 16 ambazo zitapita kwenye hatua ya mtoano.

Matokeo ya leo kwa mechi za awali za mtoano ilikuwa namna hii:-Ukonga Warriors pointi 37 v Mbagala Hard Core pointi 25, Ukonga Hitmen pointi 51 v Kigamboni City pointi 21, Oysterbay pointi 50 v Obays Finest pointi 17.

Kwemye michuano hii inayoendelea viwanja vya JMK Parks hakuna kiingilio.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic