August 26, 2019




UONGOZI wa KMC , umesema kuwa bado haujaelewa sababu za wachezaji kushindwa kupata ushindi mbele ya AS Kigali kwenye mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho uliochezwa Ijumaa, uwanja wa Taifa.

KMC ilihitaji ushindi wa aina yoyote mbele ya AS Kigali mwisho wa siku walipoteza kwa kufungwa mabao 2-1 jambo lililowafungashia virago jumla michuano ya kimataifa.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa KMC, Anwary Binde amesema kuwa hakuna jambo ambalo wachezaji hawakutimiziwa na waliahidiwa bonasi kubwa mwisho ndoto zao zimeyeyuka.

“Inaumiza kwa hatua ambayo tumeshia kwani maandalizi yalikuwa vizuri na wachezaji walituahidi kufanya vizuri kwa ajili ya Taifa mwisho wa siku tumeambulia maumivu sio kitu kizuri.

“Kwa sasa tunaacha yote yapite kwani maisha lazima yaendelee na nguvu zetu tunazipeleka kwenye maandalizi ya ligi tunaamini tutafanya vizuri, kazi kubwa tutaifanya kupata matokeo chanya mbele ya Azam FC,’ amesema Binde.

Mchezo wa kwanza wa Azam FC utakuwa Agosti 29 utakaopigwa uwanja wa Uhuru, msimu uliopita walipokutana uwanja wa Uhuru walitoka sare ya kufungana mabao 2-2.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic