August 26, 2019



MSIMU wa Ligi Kuu Bara 2019/20, umeanza  Jumamosi ambapo mechi tano zimechezwa kwenye viwanja vilivyopo kwenye mikoa mbalimbali.

  Pia hata jana pia ligi iliendelea kwa michezo miwili kuipgwa kwenye mikoa tfauti na leo ni mapumziko kwa timu kujipanga upya.

Mechi za Jumamosi Mbao ililazimisha sare ya kufungana bao 1-1 na Alliance, Mbeya City ililazimisha sare ya bila kufungana na  Prisons, Namungo ilishinda kwa mabao 2-1 mbele ya Ndanda, Polisi Tanzania ikaichapa bao 1-0 Coastal Union na Biashara United ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-0 dhidi ya Kagera Sugar.

Na jana Lipuli iliinyoosha Mtibwa Sugar kwa mabao 3-1 na Mwadui FC kuibuka na ushindi wa bao 1-0 mbele ya Singida United. 

Jambo zuri ni kwamba, kabla ya ligi haijaanza kuchezwa, tayari Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imefanya maboresho ya kanuni zake na kuziweka hadharani. 

Sasa kila timu shiriki na wadau mbalimbali wakiwemo mashabiki wa timu hizo wanazitambua sheria hizo.

Ikitokea siku timu, mchezaji au kiongozi yeyote wa timu amepewa adhabu kulingana na kosa alilolifanya kwenda kinyume na kanuni zinavyotaka, hakutakuwa na malalamiko kwa sababu vitu vipo wazi.

Kitu kikubwa pia ambacho binafsi nimeona kizuri katika hili ni namna ya kuweka wazi timu ambazo zitashuka daraja kutoka Ligi Kuu Bara baada ya kumalizika msimu huu, lakini pia njia za kuzipata timu ambazo zitapanda kutoka 

Ligi Daraja la Kwanza kucheza Ligi Kuu Bara msimu ujao wa 2020/21.

Msimu unapoanza, kila timu itakuwa inafahamu inatakiwa kufanya nini ili kuepuka janga la kushuka daraja.

Tuliona msimu uliopita ambao timu mbili za Ligi Kuu Bara zilishuka daraja moja kwa moja, huku mbili zikiponea tundu hilo baada ya kushinda mechi zake za play off.

 Sasa safari hii zinashuka timu nne moja kwa moja, kisha mbili zitacheza play off. Naamini ushindani utakuwa mkubwa sana msimu huu kwa sababu hakuna timu ambayo itacheza kinyonge ikifahamu kwamba kuanzia nafasi ya 17 hadi 20, kuna kushuka daraja.

Lakini pia ukiwa katika nafasi ya 15 na 16, utakuwa kwenye hatari ya kushuka pia kwa sababu utalazimika kucheza mechi za play off. Kushinda kwako ndiyo kutakuokoa, la sivyo unakwenda na maji.

Ni wakati sasa wa timu kuzichanga vema karata zao ili kutoa ushindani wa kweli msimu huu tofauti na ilivyokuwa msimu uliopita ambapo kuna baadhi ya mechi kabla hazijachezwa, unaweza kutabiri kwa uhakika nani atakuwa mshindi.

Tunahitaji ligi yenye ushindani mkubwa, kwa staili hii ushindani utakuwepo, lakini pia uamuzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kupunguza idadi ya timu kutoka 20 hadi 18 kwa msimu ujao, kisha timu 16 msimu ule unaofuata wa 2021/22, ni uamuzi mzuri kwani hapo itaondoa ile hali ya kushindwa kuimudu ligi yenyewe inayozalisha viporo visivyo na ulazima.

Nikiachana na Ligi Kuu Bara, nije katika hili suala la wawakilishi wetu kwenye michuano ya Shirikisho la Soka Afrika (Caf). KMC walicheza na AS Kigali baada ya mchezo wa kwanza kule Kigali nchini Rwanda kumalizika kwa matokeo ya 0-0 ukiwa ni wa Kombe la Shirikisho Afrika.

Na wametolewa kwa kufungwa mabao 2-1 uwanja wa Taifa kbala ya jana Simba nao kufungashiwa virago kwa faida ya bao la ugenini walilolipata UD do Songo baada ya kutoka sare ya kufungana bao 1-1.

 Jumamosi, Azam FC akiwa mwenyeji wa Fasil Kenema ya Ethiopia, mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika. Mechi ya kwanza kule Ethiopia, Azam alifungwa 1-0 na alishinda kwa mabao 3-1 na kupenya hatua ya inayofuata kwa jumla ya mabao 3-2.

Yanga huko Botswana ilifanya kweli mbele ya Township Rollers baada ya mchezo wa kwanza hapa nyumbani wa Ligi ya Mabingwa Afrika kumalizika kwa sare ya 1-1, wakwafungashia virago wenyeji wao kwa kuwafunga bao 1-0 ugenini.


Watanzania tukubali kwamba mpira ni dakika tisini na kuweka maneno mengi mdomoni bila vitendo hayatusaidii bali yanatupoteza.

Kupoteza kwa timu zetu nyumbani inauma lakini hakuna namna zaidi ya kujifunza kufanya vema kwa ajili ya wakati mwingine kitaifa na kimataifa.

Hivyo iwe darasa kwa wawakilishi wetu waliobaki kimataifa ambao ni Yanga kwa upande wa Ligi ya Mabingwa Afrika na Azam FC kwa upande wa Kombe la Shirikisho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic