August 21, 2019



MUSSA Mgosi, Kocha Msaidizi wa timu ya Vijana chini ya miaka 20 amesema kuwa kilichowaponza Azam FC kushindwa kupenya mbele ya Simba ni safu ya mabeki kushindwa kusoma alama za nyakati mapema pamoja na safu ya ushambuliaji kuwa na hofu.

Kwenye mchezo wa ufunguzi wa Ligi Kuu Bara ambao ni wa Ngao ya Jamii, Simba ilishinda kwa mabao 4-2 dhidi ya Azam FC kwenye mchezo wa 12 wa ngao ya jamii uliochezwa Uwanja wa Taifa.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mgosi amesema kuwa bado Azam FC ina nafasi ya kurekebisha makosa yake kwa ajili ya michuano ya Kimataifa kwani muda upo.

“Nimeutazama mchezo wa Simba dhidi ya Azam ulikuwa na ushindani mkubwa ila tatizo kubwa linaonesha kwamba bado kuna tatizo la hofu kwa washambuliaji wa timu zetu pamoja na mabeki kutokuwa makini kurekebisha makosa.

“Azam FC kwa sasa wanapeperusha Bendera ya Taifa wana kazi ya kurekebisha makosa yao waliyoyafanya ukizingatia wanashiriki michuano ya kimataifa hasa safu ya mabeki pamoja na washambuliaji kwani walipata nafasi nyingi wakashikwa na hofu ya kuzitumia,” amesema Mgosi.

Azam FC itamenyana na Fasil Kenema ya Ethiopia mchezo wa marudio kati ya Jumamosi, Uwanja wa Chamazi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic