FELIX
Minziro, Kocha Mkuu wa Singida United kwa sasa anapata taabu kweli kusuka safu
kali ya ushambuliaji kwani imekuwa ikisumbuliwa na ubutu huku safu yake ya
ulinzi ikiruhusu mabao.
Kuelekea
kwenye Ligi Kuu Bara inayotarajiwa kuanza Agosti 24, tayari Singida United
imecheza michezo ya kirafiki mitano na imeambulia kipigo kwa kukusanya jumla ya
mabao 13 huku wao wakifunga jumla ya mabao manne.
Matokeo yake yapo namna hii:- Singida United
0-1 Mashujaa, Singida United 0-4 Kagera Sugar, Singida United 1-3 Tanzania
Prison, Singida United 2-3 Mbao, Singida United 1-2 Biashara United.
Akizungumza
na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Singida United, Cales Katemana amesema
kuwa huu ni mwanzo wa kukiandaa kikosi upya wana imani ya kufanya vizuri baada
ya kugundua makosa.
“Kocha Minziro kwa sasa anapambana kusuka kikosi kipya ndio maana amekuwa akipata matokeo ambayo hayafurahishi, ila kwa sasa tayari benchi la ufundi limejua makosa ya timu kilichobaki ni kuyafanyia kazi,” amesema.
0 COMMENTS:
Post a Comment