August 26, 2019



Moja ya sakata kubwa lililotanda hivi sasa kwenye soka ni suala la ubaguzi kwa wachezaji kwenye mitandao ya kijamii.
Hasa wachezaji weusi ndio walioandamwa mno kwenye soka la England ambayo ni ligi pendwa duniani kote.

Sio suala dogo, limekuwa  kubwa kupita kiasi hadi baadhi ya makampuni ya mitandao ya kijamii imeingilia kati ili kuweza kunusuru biashara yao.

Yote hayo yanafanywa na mashabiki ambao wanaonyesha kuwa hawana simile hata kidogo, wao wanataka kufurahi tu basi.

Sasa tuje hapa kwetu Bongo, wachezaji na viongozi wa mpira wetu wanateseka kweli kwenye hiyo mitandao ya kijamii ila bahati mbaya hakuna wa kuwasaidia kupaza sauti.

Moja ya mashabiki ambao hawana nidhamu kabisa ni mashabiki wa soka la Bongo, yaani wao kukurushia matusi kwenye mitandao hawaoni shida.

Tena hawatoishia kukutukana wewe tu, bali watafika hadi kwa familia yako na hata wazazi wako nao wanamwagiwa matusi ambayo hayana msingi wowote.

Yaani ukiwa mchezaji au kiongozi kwenye soka la Bongo ujue umeyaita matusi kwako maana mashabiki wa soka wa nchi hii akili zao wanazijua wenyewe.

Lazima tuseme ukweli mashabiki wengi wa soka kwenye nchi hii hawana nidhamu hata kidogo na ndio maana wao hawaoni shida kumwaga matusi hadharani bila wasiwasi wowote.

Wenzetu mbele hasa hasa kwenye ligi za Ulaya ni rahisi kuwadhibiti mashabiki wahuni kutokana na ukubwa wa teknolojia yao, ila kwa hapa Bongo ni shida, yaani shabiki atakutukana lakini hakuna hatua yeyote itakayochukuliwa dhidi yake.

Mfano hivi sasa wanasakwa mashabiki waliotoa maneno ya kibaguzi kwa Paul Pogba wa Manchester United na nina hakika watakamatwa na sheria itafanyakazi yake lakini Bongo ndio ingekuwa ishapita hiyo.

Siku hizi ukipita kwenye mitandao ya kijamiii utaona kinachoendelea huko kejeli tu zinatawala kwa wachezaji na viongozi hasa pale timu inapofanya vibaya, lakini hawapati msaada wowote wa kisheria.

Tunajua kwetu ni ngumu sheria kufanyakazi yake kwenye hilo, lakini mashabiki basi wawe wastaarabu maana huyo mchezaji au kiongozi ni binadamu kama wewe, naye anaumia.

Ifike wakati uhuni usipewe nafasi kwenye soka letu na ndio maana kuna baadhi ya watu wamesusa hata kwenye viwanjani na kuwa karibu na mpira kwa sababu hiyohiyo ya tabia ya uhuni na wakati ndio huu wa kuondoa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic