August 25, 2019



UONGOZI wa Mtibwa Sugar umesema kuwa hautakuwa na cha msalie mtume mbele ya Lipuli kwenye mchezo wa leo utakaochezwa uwanja wa Samora.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru amesema kuwa wamefanya maandalizi makubwa kwa ajili ya msimu mpya na hesabu zao ni kushinda ugenini.

“Msimu uliopita hesabu zetu ziligoma baada ya kuteleza kidogo mwanzo ila kwa sasa tumeshajifunza na kazi inaanza rasimi mbele ya Lipuli mpaka ligi inaisha tutakuwa pale tunapohitaji, tunawapiga wakiwa kwao” amesema Kifaru.

Msimu uliopita Mtibwa ilimaliza ligi ikiwa nafasi ya tano baada ya kucheza michezo 38 na ilijikusanyia pointi 50, leo itafungua pazia kwa kuanza na Lipuli uwanja wa Samora itamkosa nahodha wao Shaban Nditi ambaye ni majeruhi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic