August 2, 2019



UNYONGE umeanza kutanda kwenye mioyo ya watanzania hasa baada ya kuona kwamba timu yao pendwa namba moja imeshindwa kupata matokeo ambayo walitarajia awali kuona inashinda kwenye ardhi ya nyumbani.

Kila mmoja ameona na kushuhudia namna timu yetu ya Taifa ilivyopambana mbele ya Kenya mchezo wa kufuzu michuano ya Chan inayotarajiwa kufanyika mwaka 2020 nchini Cameroon pale uwanja wa Taifa.

Tumekosa matokeo inabidi tukubali kwani mpaka dakika tisini zinakamilika ubao ulikuwa unasomeka Tanzania ambao ni wenyeji 0 sawa na Kenya ni matokeo ya kipekee hasa ukiwa nyumbani kwenye michuano mikubwa.

Tusisahau kwamba kwenye mpira siku zote kuna matokeo matatu ambayo ni lazima yatokee kwa namna yoyote ile wakati timu inacheza kwenye aina yoyote ya michuano hasa kwenye ulimwengu wa soka.

Ushindi, hapa kila timu na kila mwalimu anayepeleka timu yake uwanjani anaamini kwamba kipaumbele cha kwanza ni kupata matokeo chanya yatakayowapa furaha mashabiki wa timu pamoja na timu kiujumla.

Kufungwa hapa ni pale ambapo timu zote huwa hazifikirii kupoteza ila kutokana na makosa ambayo yatafanywa ndani ya uwanja yatasababisha mmoja afungwe na apoteze mchezo wake akiwa uwanjani nayo pia ni sehemu ya matokeo.

Sare hapa ndipo timu  zote mbili zimeishia kwamba hakuna mbabe aliyeibuka kidedea wote wametosahana nguvu na hakuna ambaye ameona lango la mwenzake hiyo ni matokeo ambayo yanatupa picha ya kazi mpya tuliyonayo kwenye mchezo wetu wa marudio.

Haitakuwa kazi rahisi kupenya kwao kama ambavyo tunafikiria hivyo wachezaji mna kazi kubwa ya kufanya kuelekea kwenye mchezo wa marudio utakaopigwa  Kenya Agosti 4.

Kushindana lazima kuendelee kwa wachezaji kuhakikisha kwamba wanafikia malengo ambayo waliyaweka awali na hakuna haja ya kukata tamaa kwani muda bado unaruhusu kupata matokeo chanya ugenini.

Kila kitu kinawezekana kwenye uwanja wa mpira hasa ukizingatia kwamba mpira ni sayansi na mbinu hakuna jambo jingine ambalo linabeba mafanikio kwenye mpira zaidi ya mipango makini kufikia mafanikio.

Kama ilivyokuwa kwa wenyeji wa michuano ya Afcon Misri walipoteza mbele ya Afrika Kusini nao wakawa watazamaji kama watu wengine kwenye michuano ya Afcon ambayo ilifanyika nyumbani kwao hivyo nasi tunaweza.

Kuelekea kwenye mchezo wa marudio wachezaji wanapaswa wabadili mbinu wasiende kujilinda pekee bali wafunguke kutafuta matokeo chanya hasa bila kusahau kuwa na mikakati ya kulinda na lango lao pia.

Tujipange mwanzo mwisho huku tukiamini kwamba hakuna jambo baya kama kukata tamaa mapema kabla hata mchezo haujachezwa tuamini kwamba uwezo wetu ni mkubwa na wachezaji wetu tayari wameshaanza kuzoena  pamoja na kujua kile ambacho wanatakiwa kukifanya.

Ninaamini sare waliyopata nyumbani si  matokeo mabaya ambayo yanapaswa kubezwa wamejitahidi kwa kiasi chake wachezaji wetu licha ya kwamba hesabu zetu ilikuwa ni kupata ushindi.

Kinachotakiwa kwa sasa ni kurekebisha makosa ambayo tumeyafanya mwanzo kwenye mchezo wetu wa nyumbani na kwenda tukiwa na mipango mipya ya kupata matokeo ugenini nafasi yetu ya kushinda ndio hii.

Kujiamini kwa wachezaji kutasaidia kubadili mbinu pia na kuwafanya wacheze kwa kujituma mwanzo mwisho hivyo wanapswa wajengwe kisasikolojia kujega muunganiko mzuri na makini huku malengo makubwa ikiwa ni kufuzu kushiriki Chan.

Yatupasa kujua kwamba nini tumekifuata nchini Kenya na kujituma kwa kupambana hasa katika mchezo wetu wa marudo ambao ni muhimu kwetu kushinda ili kusonga mbele kawenye michuano hii ambayo inawahusu wachezaji wa ndani.

Benchi la ufundi nina amini limeona mapungufu ya timu yetu na kuyafanyia kazi ili kupata matokeo mazuri kwenye mchezo wa marudio tunaamini kwamba bado mashabiki wapo bega kwa bega na timu ya Taifa hivyo ni suala la kusubiri na kuona nini kitatokea.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic