KAZI imeanza
ya kuisaka tiketi kwa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kupiga hatua
mpaka kwenye Kombe la Dunia linalotarajiwa kufanyika mwaka 2022 nchini Qatar
hasa baada ya michezo ya awali kuanza kuchezwa.
Hakika kwa
sasa wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ wana kibarua kizito
mbele ya Burundi baada ya kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 wakiwa ugenini.
Kwenye
mchezo wa kwanza wa kufuzu hatua ya makundi uliochezwa nchini Burundi, Jumatano haikuwa
rahisi kwa Stars kupata matokeo hayo kutokana na kushindwa kutumia nafasi za
wazi ambazo walizitegeneza.
Pia
ikumbukwe Stars ilikuwa ugenini kuna ugonjwa wa hofu ya uwanja ambao ulikuwa
unawamaliza hasa dakika za mwanzo kwa kushindwa kuwa makini jambo lililopelekea
sare ya kufungana bao 1-1.
Kwa hapo
ambapo mabalozi wetu wamefanya wanastahili pongezi kwani wamevuna kile ambacho
walikipanda na walistahili kutokana na juhudi ambazo walizionyesha bila kukata
tamaa licha ya kuwa nyuma kwa bao moja.
Hapo kuna
somo kubwa la kujifunza kwa wachezaji pamoja na benchi la ufundi kwamba uwezo
wa kuwafunga Burundi tunao nao pia wana uwezo wa kutufunga endapo tutashindwa
kuwa makini.
Kikubwa
ambacho kwa sasa inabidi kitazamwe kwa umakini na ukaribu ni mchezo wamarudio
unaotarajiwa kuchezwa Septemba nane uwanja wa Taifa.
Wachezaji kwa
hapo nini tena mnataka kwa sasa zaidi ya kutoa burudani kwa mashabiki? Ukizingatia
uwanja ni wa kwenu nanyi mpo kwenye himaya yenu kinachotakiwa ni ushindi wa
mapema na kufunga hesabu.
Matokeo
ambayo yametokea Burundi piga ua huwezi kuyabadili abadani zaidi ya kubaki
stori sasa kinachotakiwa kubadilishwa kwa sasa ni mfumo wa kufikiria kwa
wachezaji wetu.
Wachezaji
wetu wote wanapaswa wafikirie kwamba wanakutana na mchezo mgumu ambao unahitaji
nidhamu ya hali ya juu pamoja na umakini.
Maelekezo ya
benchi la ufundi pamoja na wale wachezaji wa zamani ambao wamekuwa wakisafiri
na timu yakitendewa kazi kwa ufasaha basi kazi inakuwa imeisha mapema kabisa.
Kitu kikubwa
kwa wachezaji kubadili mbinu zao ambazo walizitumia awali kwa kushindwa kuwa na
maamuzi ya haraka hasa wanapokuwa karibu na eneo la hatari pamoja na kupoteza
mipira kizembe.
Kazi ya
kucheza na timu ambayo falsafa zinalingana ni ngumu kwani mbinu zote zinakuwa
mikononi mwa wapinzani sasa ili kupenya kundi la namna hiyo akili ya ziada
inahitajika bila kusahau juhudi.
Uwepo wa
mashabiki ndani ya uwanja wa Taifa iwe ni silaha ya mwisho ya maangamizi kwa
wapinzani wetu kwani kama ambavyo wao walikuwa wanajivunia nguvu ya mashabiki
kwao basi sisi tuifanye kama silaha ya mwisho ili kuwapoteza jumla.
Mashabiki
wote ni wakati wa kuungana kwa ajili ya Taifa Stars ili ipate matokeo chanya
yatakayoipa nafasi ya kusonga mbele na kutinga hatua ya makundi kwenye michuano
ya Kombe la Dunia.
Sio kazi
nyepesi ingawa timu itakuwa nyumbani ni mpaka pale wachezaji wenyewe watakuwa
na nia moja na kushirikiana katika kila hatua.
Ule ugumu wa
kushindwa kuamua pamoja na uzembe usio na lazima ndani ya uwanja uishie kwenye
mazoezi ndani ya uwanja ni kazi juu ya kazi mpaka kupata matokeo.
Kila la
kheri Taifa Stars watanzania na wadau wote wanawatazama nyie kuona ni namna
gani mtafikia yale malengo ya Taifa na timu kiujumla.
Furaha ya
mashabiki imejificha kwenye matokeo na wenye kuamua matokeo ndani ya uwanja ni
wachezaji ambao mmepewa dhamana ya kupeperusha bendera ya Taifa kimataifa, msiwaangushe
watanzania.







0 COMMENTS:
Post a Comment