September 9, 2019



UONGOZI wa Mtibwa Sugar umesema kuwa kwa sasa hesabu zoa kubwa ni kupata pointi tatu muhimu mbele ya Simba mchezo unaotarajiwa kuchezwa Septemba 17 uwanja wa Uhuru.

Mtibwa Sugar walipoteza mchezo wa kwanza kwa kufungwa mabao 3-1 dhidi ya Lipuli FC itamenyana na Simba ambayo ilishinda mabao 3-1 mbele ya JKT Tanzania uwanja wa Uhuru.

Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru amesema kuwa wanawaheshimu wapinzani wao Simba ila wanachohitaji ni pointi tatu.

“Mchezo wa kwanza tulipoteza mbele ya Lipuli sasa ni muhimu kwetu kushinda mchezo wetu wa Simba tunahitaji kupata pointi tatu zao ili kujiweka kwenye mazingira ya ushindani.

“Kushindana na timu bora ni jadi yetu kwani nasi tuna kikosi bora chenye uwezo wa kupambana mashabiki watupe sapoti ya kutosha kupata burudani,” amesema Kifaru.

2 COMMENTS:

  1. mmejipa kazi ngumu mtusamehe tafuteni baadae point tatu au subirini ile timu yenu maana na sisi tunajua mbeleni tunawababe wetu

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic