September 3, 2019



UONGOZI wa Ruvu Shooting umesema kuwa msimu huu wa mwaka 2019/20 wamejipanga kuushangaza ulimwengu wa mpira kwa kutwaa kombe la ligi lililo mkononi mwa Simba.

 Ruvu Shoting ilishinda mchezo wake wa kwanza mbele ya Yanga ikiwa ugenini kwa ushindi wa bao 1-0 na kuvunja rekodi iliyodumu kwa muda wa misimu 9 ambapo Ruvu Shooting ilikutana na Yanga mara 18 na ilipoteza jumla ya mechi 15 na sare tatu.

Bao pekee lililoipa ushindi Ruvu Shooting lilipachikwa kimiani na Sadat Mohamed akimalizia pasi ya Hassan Dilunga, uwanja wa Uhuru.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire amesema kuwa wamejipanga kufanya maajabu ambayo yatashangaza ulimwengu kwa kutwaa kombe la ligi.

“Hapa hakuna cha Simba wala Yanga, kazi ndo imeanza kwa sasa hawa Yanga tuliwaambia wameponzwa na ubishi wao ni salamu kwa walioshikilia ubingwa kwamba mwendo wetu mpaka tunautwaa ubingwa msimu huu,” amesema Bwire.



1 COMMENTS:

  1. Lugha kama hiyo waliitumia Yanga dhidi yenu na leo unaitumia Kwa wengineo. Ni mspema Sana kutamba usubiri kidogo kwasababu Kiki ndio inaanza. Mwaka Jana Mbao, Mtibwa na Azam waliongoza vizuri mwanzoni

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic