FRED
Minziro, ‘Baba Isaya’ aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu ya Singida United amesema
kuwa alishasoma alama za nyakati ndani ya Singida United zilizompa taa nyekundu
jambo ambalo halijamshangaza kuskia ametangazwa kocha mpya.
Miziro aliinusuru
Singida United kushuka daraja msimu uliopita wa mwaka 2018/19 ilimaliza ligi
ikiwa nafasi ya 13 baada ya kujikusanyia pointi 46 ilishinda michezo 11 na
kutoa sare 13 na kupoteza jumla ya michezo 14.
Minziro
amesema kuwa kupigwa kwake chini kisha Ramadhan Nsanzurwimo kurithi mikoba yake halijamshtua.
“Unajua
wengi hawaelewi namna mambo yanavyokwenda kwenye soka letu la Bongo, ila hilo
halinipi presha kwani wao wanaendelea na mambo yao nami ninaendelea na mambo
yangu.
“Kwa
mwenendo ambao nilikuwa naenda nao nilitambua kitakachotokea na kuna baadhi ya
mechi niliziacha kama ile ya Namungo sikuwepo kabisa, yote kheri maisha lazima
yaendelee,” amesema Minziro.
0 COMMENTS:
Post a Comment