October 21, 2019


Mashabiki wa Simba hivi sasa wana jeuri sana. Ukikaa pale klabuni Msimbazi utacheka sana. Jeuri yao imepitiliza hadi kufikia hatua ya kuitaka Bodi ya Ligi Tanzania (TPLB) na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kuwapangia wacheze mechi mbili kwa siku moja.

Si unafahamu kwamba  Jumatano ya wiki hii  yaani Oktoba 23, mwaka  huu wanacheza na Azam FC  pale Uwanja wa Uhuru, basi siku hiyohiyo pia wanataka  wacheze na Yanga. Wanaona Januari 4, mwakani ni mbali  sana.

Wanawataka mapema 

Ukiangalia kwenye Ligi  Kuu Bara, Simba ndiyo  vinara wa ligi hiyo wakiwa  na pointi 12 baada ya  kucheza mechi nne na  kushinda zote.

Wao na Azam  ambao wanashika nafasi  ya pili, peke yao ndiyo  wameshinda mechi zote  walizocheza hadi sasa. Azam  wamecheza mechi tatu na  kushinda zote.

Sasa  vikosi hivyo  ambavyo wanatamba navyo  Simba kwamba vina uwezo  wa kucheza mechi viwanja  tofauti kwa siku moja na  kushinda bila ya wasiwasi ni  hivi hapa:

SIMBA VS YANGA

Wenyewe wanasema mchezo  huu uchezwe Uwanja wa  Taifa jijini Dar. Kikosi ambacho kitacheza  dhidi ya Yanga wanataka  Aishi Manula akae langoni.

Shomary Kapombe,  Mohammed Hussein,  Erasto Nyoni, Pascal Wawa  wasimamie ulinzi huku  pale kati wakiwapanga  Jonas Mkude na Clatous  Chama. Mastaa wengine  waliowaweka kwenye kikosi  hiki ni Mzamiru Yassin, John  Bocco, Meddie Kagere na  Hassan Dilunga.

Katika kikosi hicho,  wachezaji wote hao  walikuwa Simba msimu uliopita na bado  anaendelea kupambana  kuhakikisha wanatetea  ubingwa wao wa Ligi Kuu  Bara. Wanaamini kwamba  kikosi hicho kinaweza  kuisimamisha Yanga bila  presha yoyote kwenye  Uwanja wa Taifa.

SIMBA VS AZAM

Uwanja wa Azam Complex  uliopo Chamazi jijini  Dar, mashabiki wa Simba  wanasema wataenda na  kikosi hiki siku hiyohiyo ya  Jumatano:

Beno Kakolanya,  Haruna Shamte, Gadiel  Michael, Kennedy Juma,  Tairone Santos, Gerson
Vieira, Deo Kanda, Sharaf  Shiboub, Miraj Athuman,  Ibrahim Ajibu na Francis  Kahata. Hapo kuna  wengine kibao wako benchi  wakiwemo vijana.

Kikosi hiki  wanachotamba kwamba  kinawatosha Azam,  kinajumuisha wachezaji wapya waliosajiliwa na  Simba msimu huu na ambao  wanafanya vizuri kila  wanapopewa nafasi.

Ni mashine ambazo lengo  la Kocha na uongozi wa  Simba ilikuwa kuwatumia  kuongeza nguvu kwenye  michuano ya kimataifa  ambayo walitolewa mapema  bila kutarajia.

6 COMMENTS:

  1. Simba wapo vizuri ila kujiamini kuliko kiasi kutawatumbukia nyongo kwani tayari walishachemsha kwa Du Songo ya Msumbiji kimzaha mzaha. Wafahamu hata Manchester city hufungwa na vitimu vya hovyo kabisa . Kwa hivyo waache kujigamba na ukubwa wa kikosi bali wanatakiwa kujipanga.

    ReplyDelete
  2. unaweza kuchangia hoja au kutoa maoni kwakutumia kichwa cha habari?yani ametumia kichwa cha habari kucoment pole sana brother,ila tambua tu simba hawajaongea hivyo hao ni mashabiki wa simba.

    ReplyDelete
  3. Bado hujawataja akina Ndemla , Mlipili , Rashid juma , Wilker Da Silver

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic