November 9, 2019



PATRICK Aussems, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa alistahili kupata sare ya bila kufungana na Tanzania Prisons ya Mbeya kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara kutokana na kikosi hicho kuwa na mbinu za kiufundi mwanzo mwisho.

Simba ambao ni mabingwa watetezi wa ligi Novemba 7 ilikubali kupata sare ya bila kufungana na Prisons kwenye mchezo wake wa tisa wa ligi uliochezwa uwanja wa Uhuru.

Aussems amesema kuwa Prisons ilifanikiwa kuwa na ukuta mgumu ambao ulikuwa ukizuia mipango ya wachezaji wake wa Simba na ilikuwa ikifanya mashambulizi ya kushtukiza na kurejea kwenye nafasi zao kwa wakati kwa kila mchezaji.

"Kazi kubwa ambayo wachezaji walikuwa wakifanya ilikuwa ni kupambana na timu ambayo ilijipanga kujilida na kushambulia kwa kushtukiza jambo ambalo limetufanya tusipate ushindi.

"Nawapongeza wapinzani wetu kwa kupambana na kupata sare licha ya wachezaji wangu kupambana kutafuta ushindi, ni wakati wetu kujipanga kwa ajili ya wakati mwingine," amesema.

Sare hiyo inaifanya Simba kufikisha jumla ya pointi 22 ikijikita kileleni huku Prisons ikiendeleza rekodi yake ya kutokupoteza mchezo ndani ya ligi baada ya kucheza mechi 10 ikiwa na pointi 16 imetoa sare mechi saba na kushinda mechi tatu inashika nafasi ya nne kwenye msimamo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic