December 10, 2019


Kocha wa zamani wa Yanga, Hans Pluijm amethibitisha kutuma barua ya kuomba kazi ndani ya timu hiyo wiki mbili zilizopita kurithi mikoba ya Mwinyi Zahera aliyetimuliwa mwezi uliopita. Imeelezwa.

Zahera ambaye kwa sasa yupo hapa nchini kudai stahiki zake alifungashiwa virago baada ya timu hiyo kuboronga kwenye mechi za kimataifa na zile za Ligi Kuu Tanzania Bara na kikosi hicho kukabidhiwa kocha wa muda Charles Mkwasa.

Pluijm aliyekinoa kikosi hicho kwa mafanikio makubwa kwa misimu ya nyuma na kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara alisema licha ya mambo yanayoendelea kwenye timu hiyo ikiwemo baadhi ya wachezaji kuhusishwa kuondoka kutokana na matatizo ya stahiki zao haimkatishi tamaa.

Taarifa imesema kuwa, Hans amethibitisha hilo na kudai hadi sasa mipango ya mawasiliano na uongozi wa timu hiyo inaenda vyema .

Imeenda mbali kwa kueleza wakati anakinoa kikosi hicho alikuwa anafanya kazi kwa uhuru mkubwa ikiwemo kupata ukarimu kutoka kwa mashabiki na ushirikiano kutoka kwa viongozi sambamba na wachezaji hadi kupata mafanikio na hicho ndicho kinachozidi kumpa nguvu ya kuomba kazi tena kwenye timu hiyo.

1 COMMENTS:

  1. Mabadiliko ya Uendeshaji na kuifanya timu kuingia kwenye uwekezaji .....NINASHANGAA M/KITI ANASEMA ILE KAMATI ILIYOUNDWA INAENDELEA NA MCHAKATO KUTOKA MWAKA JUZI IMEKUWA NA VIKAO VINGI SANA YAANI WANASEMA MPAKA MWAKANI MWEZI WA 6....SASA WATAKUWA WAMECHUKUA MWAKA. 1 1/2...HUKU MNALIA GHARAMA ZA UENDESHAJI NA MAPATO HAYALINGANI NA MATUMIZI........MNATEGEMEA KUONGEZA WANACHAMA KUANDIKISHA WANACHAMA ILI MPATE FEES ILI ZIENDESHE KLABU KUBWA KAMA YANGA??? DAWA NI KUINGIA UBIA/UWEKEZAJI NDANI YA SIKU 60 HAKUNA MUDA WA KUSUBIRI KWAKUWA MMESHAPOTEZA MUDA MWINGI KATIKA MICHAKATO....KUNA VITU VINATAKIWA MITAJI MIKUBWA YA FEDHA KAMA USAJILI, KAMBI, POSHO, UJENZI WA VIWANJA VYA MAZOEZI (KIGAMBONI & KAUNDA) AMBAPO NI MATAJIRI WENYE UWEZO WA KIFEDHA WANAWEZA KUTATUA HILI.....MSIWE NA MAWAZO YA KARNE YA 18...KUTAFUTA MICHANGO KUTOKANA NA KUINGIZA WANACHAMA WAPYA HIZO NI NDOTO HAMUWEZI KUFANIKIWA...100% WANACHAMA KULIPA MICHANGO HAWAWEZI.....KUTOKANA NA UHALISIA WA UCHUMI UNAOBADILIKA KWA KASI

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic