February 23, 2020


TIMU ya KMC imeacha pointi sita jumla ugenini kwenye mechi zake mbili ilizokuwa ikicheza nyanda za juu Kusini.

KMC ilianza kupoteza mbele ya Namungo FC Uwanja wa Majaliwa kwa kufungwa mabao 2-1 kisha ikafuata kupoteza mbele ya Ndanda FC Uwanja wa Nangwanda Sijaona kwa kufungwa mabao 2-1.

KMC imekubali kufungwa mabao manne huku wao wakishinda mabao mawili kwenye mechi mbili walizocheza.

Wafungaji wa mabao ya KMC ni James Msuva na Mohamed Samatta.

Kwenye ushindi wa Ndanda SC wa mabao 2-1 mbele ya KMC FC mabao yalifungwa na Kiggi Makasi  dakika ya 2 na Abdulrazack Ramadhan dakika ya 70 na lile la KMC likifungwa na Mohamed Samatta dakika ya 77

1 COMMENTS:

  1. Lindi na mtwara ni kanda ya kusini@Saleh....si Nyanda za juu kusini tafadhali

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic