NYOTA wa
kigeni ndani ya kikosi cha Simba wameonekana na balaa kwenye kucheka na nyavu
huku wakiwapoteza wazawa ndani ya kikosi hicho cha Mabingwa watetezi wa Ligi
Kuu Bara.
Simba ikiwa
ipo nafasi ya kwanza kwenye msimamo baada ya kucheza mechi 28 imefunga mabao 63
ambapo wazawa wamefunga mabao 22 na wageni wamefunga mabao 41 wakiwapoteza pia wafngaji wa Yanga ambao jumla wametupia mabao 31 kwenye mechi 27.
Kinara wa
kutupia mabao kwa wageni ambaye pia anakimbiza kwenye ligi ni Meddie Kagere
raia wa Rwanda mwenye mabao 19 akifuatiwa na Deo Kanda raia wa Congo mwenye
mabao 7, Francis Kahata raia wa Kenya ametupia mabao manne huku Lusi Miqussone
raia wa Msumbuji, Gerson Fraga raia wa Brazil
wakitupia mabao matatumatatu kila mmoja.
Sharaf Shiboub raia wa Sudan na Clatous Chama
raia wa Zambia wakitupia mabao mawilimawili, Tairone Santos raia wa Brazil ametupia bao moja.
Kwa upande wa Yanga mgeni anayekimbiza kwa kutupia ni David Molinga mwenye mabao nane akifuatiwa na Patrick Sibomana mwenye mabao matano huku Bernard Morrison akitupia mabao matatu, Haruna Niyonzima, Yikpe hawa wametupia bao mojamoja.
Kwa upande
wa wazawa ndani ya Simba, Miraj Athuman ‘Sheva’ na Hassan Dilunga wanaongoza jahazi kwa kutupia
mabao sita kila mmoja wakifuatiwa na nahodha John Bocco mwenye mabao manne,
Jonas Mkude na Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ wametupia mabao mawilimawili huku Ibrahim
Ajibu na Erasto Nyoni wakitupia bao mojamoja.
Huyo ndio mwamba wa lusaka
ReplyDelete