OBREY
Chirwa, mshambuliaji namba moja wa Azam FC anawaongoza washambuliaji wenzake watatu
kwenye kuvunja rekodi zao walizoweka msimu uliopita kibabe.
Chirwa msimu
wake wa kwanza ndani ya Azam FC 2018/19 akiwa ni ingizo la dirisha dogo
alitupia mabao matatu na msimu huu ametupia mabao nane.
Wengine
ambao wamevunja rekodi zao kibabe ni pamoja na Paul Nonga anayekipiga Lipuli,
msimu uliopita alifunga mabao matano msimu huu ametupia mabao 11 akiwa ndani ya
Lipuli.
Yusuph Mhilu
akiwa Ndanda alitupia mabao matatu msimu huu akiwa ndani ya Kagera Sugar
ametupia mabao 11.
Bigirimana
Blaise akiwa Stand United msimu uliopita alitupia mabao 10 msimu huu akiwa
Namungo ametupia mabao 10 na kuifikia rekodi yake aliyoiweka msimu uliopita.
0 COMMENTS:
Post a Comment