June 24, 2020




MTENDAJI Mkuu wa Azam Media, Tido Mhando, jana amezindua rasmi tamthilia nne ambazo zitarushwa kwenye Chanel 103 ya Sinema zetu ukiwa ni mpango endelevu wa kuleta ushindani kwenye masuala ya filamu kitaifa na kimataifa.

Uzinduzi huo ulifanyika kwenye Ukumbi wa Hotel ya Kilimanjaro, ulihudhuriwa na waigizaji wakongwe na chipukizi ambao walicheza kwenye tamthilia hizo.

Mhando alisema, tamthilia hizo nne ni pamoja na Shilingi iliyozalishwa  na kampuni ya Omary Film Ltd na Tandi iliyozalishwa na kampuni ya JK Production ambazo zitarushwa siku ya Ijumaa na Jumapili majira ya saa 3 usiku kuanzia Julai 17.

Panguso iliyozalishwa na kampuni ya Wateule Inc na Single Mama iliyozalishwa na JB Film Company zitaonyeshwa kuanzia Jumatatu mpaka Alhamisi, kuanzia Julai 13.

Mhando amesema:-"Tunarejea upya na tulianza mpango huu kuupanga tangu mwishoni mwa mwaka 2019 na sasa kazi imeanza.

" Malengo makubwa ya Azam TV ni kuona kwamba tunaweza kushindana na wenzentu walioanza ikiwa ni wale wa Ghana na Nigeria na inawezekana kwa kuwa nia ipo, na wote ambao tunafanya nao kazi ni wazawa wenye vipaji.”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic