HAYA hapa matokeo ya mechi za leo zilizochezwa za Ligi Kuu Tanzania Bara, hali ya Singida United bado ni tete, yapokea kichapo tena mbele ya Mtibwa Sugar:-
Ruvu Shooting 0-0 Ndanda SC, Uwanja wa Mabatini.
Mbao FC 1-0 Coastal Union bao limepachikwa na Jordan John dakika ya 6 Uwanja wa Kirumba.
Mwadui FC 3-0 Lipuli FC mabao yamejazwa kimiani na Isihaka Kauju dk 26 alijifunga, Wallace Kiango dakika ya 66 na Omary Daga dk 83 Uwanja wa Kambarage.
Singida United 1-3 Mtibwa Sugar watupiaji ni Ramadhani Hashim dk ya 87 kwa Singida United, Boban Zirintusa dakika ya 7 na 25’, Riphat Msuya dakika ya 64 kwa Mtibwa Sugar, Uwanja wa Liti.
Tanzania Prisons 2-2 JKT Tanzania kwa Prisons ni Adily Buha 47’ na Jeremiah Juma 83’ | Michael Aidan 16’, Mohamed Rashid 68' kwa JKT Tanzania.
0 COMMENTS:
Post a Comment