Ligi
Kuu ya Vodacom inatarajiwa kuendelea mwishoni mwa wiki kwa viwanja sita kutimua
vumbi, michezo mitatu ikifanyika siku ya jumamosi na michezo mingine mitatu
kufanyika siku ya jumapili.
Katika
Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, wenyeji timu ya Polisi Morogoro
watawakaribisha maafande wa Ruvu Shooting kutoka Mlandizi, Coastal Union
watakua wenyeji wa Kagera Sugar kwenye dimba la Mkwakwani, huku JKT Ruvu
wakiwakaribisha Azam FC katika uwanja wa Azam Complex Chamazi.
Jumapili
Mgambo JKT watakua wenyeji wa timu ya Ndanda FC kwenye Uwanja wa Mkwakwani
jijini Tanga, huku Mtibwa Sugar wakiwa wenyeji wa wagonga nyundo timu ya Mbeya
City katika Uwanja wa Manungu Turiani.
Katika
Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam watani wa jadi Simba SC watakuwa wenyeji
wa Young Africans, mchezo unaotarajiwa kuanzakutimua vumbi majira ya saa 10
kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
Jumapili
Mgambo JKT watakua wenyeji wa timu ya Ndanda FC kwenye Uwanja wa Mkwakwani
jijini Tanga, huku Mtibwa Sugar wakiwa wenyeji wa wagonga nyundo timu ya Mbeya
City katika Uwanja wa Manungu Turiani.
Katika
Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam watani wa jadi Simba SC watakuwa wenyeji
wa Young Africans, mchezo unaotarajiwa kuanzakutimua vumbi majira ya saa 10
kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
0 COMMENTS:
Post a Comment