September 2, 2020


 BAADA ya dirisha la usajili la Ligi Kuu Bara kufungwa rasmi Agosti 31 mwaka huu, aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Aden Rage amesema kuwa Tuisila Kisinda ataleta upinzani kwenye ligi.

 

Simba na Yanga zimeonyesha kuimarika katika usajili wa msimu huu hasa kuleta wachezaji wenye viwango kutoka nje na wenye majina ambao wanatarajia kuleta ushindani wa hali ya juu msimu ujao.


Simba imesajili wachezaji wanne wa kimataifa ambao ni Larry Bwalya, Bernard Morrison, Chris Mugalu na Joash Onyango, huku Yanga ikiwasajili Tuisila Kisinda, Mukoko Tunombe, Michael Sarpong, Yacoub Sogne na Carlos Stenio ‘Carlinhos’.

 

Akizungumza na Championi Jumatano, Rage alisema kuwa, Simba na Yanga zimefanya mapinduzi makubwa msimu huu kwa kusajili wachezaji nyota wenye majina hivyo ana imani kubwa ushindani utakuwa mkubwa katika ligi msimu ujao.


“Nazipongeza Simba, Yanga na Azam zimefanya usajili mzuri sana kuelekea msimu ujao wa ligi kuu, kwani timu zote zimesajili wachezaji nyota wazuri hivyo naamini msimu ujao kutakuwa na ushindani mkubwa sana kwenye ligi.


4 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic