April 10, 2021


 


KIUNGO  mshambuliaji wa Yanga, Mrundi, Saido Ntibazonkiza amepewa jukumu zito na kaimu kocha mkuu wa  timu hiyo, Juma Mwambusi  kwa  kuhakikisha anapambana na wachezaji wenzake kuisaidia timu hiyo kuchukua ubingwa msimu huu.

 

 Mwambusi  leo Jumamosi ataiongoza Yanga  katika mchezo wake wa kwanza akiwa kaimu kocha mkuu dhidi ya KMC ya katika mchezo unaotarajia kupigwa kwenye Uwanja wa  Benjamini mkapa huku ukiwa ni mchezo wake wa kwanza baada kufukuzwa kwa aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo, Cedric Kaze.

 

 Kwa mujibu wa taarifa ambazo tumezipata kutoka  ndani  timu hiyo zinasema kuwa kiungo huyo ni mmoja ya kati ya wachezaji waliopewa majukumu makubwa na kocha huyo kwa kuhakikisha wanafanikiwa kutwaa ubingwa wa msimu licha ya kupinzani mkali kutoka kwa Simba.

 

 “Mikakati imekuwa mingi sana kwa kuwa timu inataka kupata ubingwa na ndiyo limekuwa lengo kubwa kwa sasa maana wapo wachezaji waliotakiwa wabadilike na wapo waliopewa majukumu kutokana na uzoefu wao.

 

“Sasa mtu Ntibazonkiza kocha ametaka kwanza kujitoa na kuendelea kuwa kiongozi ndani na nje ya uwanja kutokana na uzoefu wake  lakini kuhakikisha Yanga inapata matokeo zaidi katika kila mchezo ambao itacheza.” Amesema mtoa taarifa.

 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic