April 8, 2021

 


MABOSI wa Liverpool wamemuambia mshambuliaji wao Mohamed Salah kuwa anaweza kuondoka hapo ikiwa atapata ofa nzuri.


Nyota huyo raia wa Misri amekuwa akihusishwa kujiunga na Klabu ya Real Madrid na Barcelona ambazo zinatajwa kuwania saini yake.


Mpaka sasa ametupia jumla ya mabao 27 kwenye michuano yote msimu huu akiwa ni namba moja kwa kucheka na nyavu katika kikosi hicho.


Kocha Mkuu wa Liverpool,  Jurgen Klopp hivi karibuni alinukuliwa akisema kuwa Salah ni miongoni mwa wachezaji muhimu hivyo ikitokea kuna timu itamhitaji ni lazima imgharamie.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic