April 17, 2021


JUNIOR Lokosa, mshambuliaji aliyesajiliwa na Simba kwa ajili ya mashindano ya kimataifa amepata warithi wake kwenye Ligi ya Mabingwa ambao ni Chris Mugalu, Meddie Kagere na John Bocco.

Lokosa raia wa Nigeria alisajiliwa na Simba akitokea Klabu ya Esperance ya Tunisia Januari, mwaka huu ila kwa sasa tayari ameshasepa Bongo kutokana na uwezo wake kuwa chini ya matarajio ya benchi la ufundi la Simba.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Kocha Mkuu wa Simba, Didier Gomes, raia wa Ufaransa alisema kuwa hana mashaka kuhusu kutokuwepo kwa Lokosa kwa sababu anao wachezaji wengine katika nafasi hiyo.

“Kwa kweli nimezungumza sana kuhusu Lokosa,(Junior) ila ngoja niweke wazi kuwa kwa nafasi ambayo anacheza wapo wachezaji wenye uwezo wa kufanya vizuri, yupo Mugalu, (Chris), Kagere, (Meddie) na Bocco, (John).

“Kikubwa ambacho ninafurahi ni kwamba wachezaji wote waliopo wanafanya kile ambacho ninawaelekeza na wanakifuata kwa wakati,” alisema Gomes. 

 


4 COMMENTS:

  1. Hapo ndo Kiswahili kinapokuwa kigumu, wanarithije mikoba ya Lokosa wakati Lokosa hakuwahi kuwa na nafasi Simba!

    ReplyDelete
  2. hv hii blog wanaoandika habar ni wamesoma kweli? kichwa cha habar tofqut kabisa na habar

    ReplyDelete
  3. Hawana kitu cha maana cha kuripoti na hivo kupelekea kuandika utumbo. Tuwasamehe bure

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic