June 20, 2021


UONGOZI wa Azam FC umeweka wazi kwamba upo tayari kwa ajili ya mchezo wao wa ligi dhidi ya Namungo FC utakaochezwa kesho, Uwanja wa Majaliwa.

Azam FC inayonolewa na Kocha Mkuu, George Lwandamina ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 63 baada ya kucheza jumla ya mechi 31.

Mchezo wa kwanza walipokutana Uwanja wa Azam Complex ubao ulisoma Azam FC 2-2 Namungo hivyo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Zakaria Thabit, Ofisa Habari wa Azam FC amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mechi zote zijazo hivyo watapambana kupata pointi tatu. 

Ikumbukwe kwamba Azam FC imetoka kushinda kwa mabao 4-1 dhidi ya Gwambina FC kwenye mchezowa ligi uliochezwa Uwanja wa Azam Complex.

Mpiana Monzizi na Idd Seleman nyota hawa walitupia mabao mawilimawili kila mmoja.

1 COMMENTS:

  1. Azam mwenye point 63 awe wapili, mwenye 64 yuko nafasi gani?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic