July 28, 2021

BAADA ya Simba SC kutwaa ubingwa mara mbili mfululizo katika Kombe la FA, huku wakiitawala Ligi Kuu kwa kutwaa makombe kwa misimu manne mfululizo, Mjumbe wa Bodi ya Utendaji ya Simba Zakaria Hans Pope ameibuka na kusema kuwa sasa mipango yao yote ni kuchukua ubingwa  katika michezo ya kimataifa.

Simba imefanikiwa kufikisha idadi ya ubingwa mara nne mfululizo katika Ligi Kuu Bara hadi sasa pia imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Shirikisho la Azam mara tatu.

Akizungumzia mipango yao, Hans Pope amesema kuwa kwa ubingwa walionao sasa unatosha kudhidirisha kuwa wao ndio mabingwa wa nchi, na wanahitaji kupata ubingwa huo hata katika michezo ya kimataifa.

“Simba ni timu kubwa kwa sasa na ndio mabingwa wa nchi kwa kuwa tumeshachukua makombe ya Ligi Kuu mara nne, na sasa tumechukua Kombe la FA kwa mara ya tatu tayari inatosha kuonyesha ukubwa wetu.

“Tunachokitaka kwa sasa ni kuvuka mipaka na kuchukua ubingwa katika mashindano mbalimbali ya kimataifa tumeshachukua sana huku nyumbani, na tumezoea ubingwa wa nyumbani hivyo kwa sasa ni levo nyingine za kimataifa na kuonyesha ukubwa wa Simba,”amesema Hans Pope.


20 COMMENTS:

  1. Baada ya manara sasa pip nae kawa msemaji wa timu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Timu ipi? Timu ya Familia? Wapenzi wa Mikia aka vichupi FC mchokezeni Barbra mwone kama hamtatimuliwa wote mrudi pale kwenye jengo lenu msimbazi mkauze vijana.

      Delete
    2. Mkauze vijora

      Delete
  2. Angeongea mwingine lkn huyu???????

    ReplyDelete
  3. Hanspooe ni Simba Damu mwengine yote semeni. Miongoni mwa wanasimba wanaoishi katika vipindi vya Raha na ziki na kamwe hatujamsikia na kauli za kutetereka juu ya mapenzi yake zidi ya simba. Ni mtu wa kujitoa kwa ajili ya Simba pia. Yanga kitu kinachowayumbisha kwa Muda Sasa ni kukosa watu Kama akina Hanspooe ndani Yanga.Kwa bahati nzuri Simba wamebahatika kuwa na hawa watu na wanasimba wanatakiwa kuwaenzi na kutambua mchango wao ndani ya simba. Watu kama Salum Abdalla try again,Akina Magori, akina Nghambi,akina kassim Dewji na wengine kadhaa nyuma ya pazia bila ya kmsahau mtendaji mkuu wa bodi ya wakurugenzi na Muekezaji Mohammed Dewji. Kuwepo watu kama akina Magori ndio bila Shaka waliowezesha kumshawishi Mo kuekeza ndani ya Simba kwa hivyo utaona umuhimu wa watu fulani katika muunganiko wa Mambo.Na hizi jitihada zao sio kwa ajili ya Simba tu bali nchi yetu kwa ujumla. Klabu zetu zikiwa zitaendelea kufanya vizuri basi hata wauza magazeti mitaani watafanya vizuri pia na media industry kwa jumla,tuamke katika kujenga vilivyo bora na kuwatia moyo wale wanaopambana katika maboresho.

    ReplyDelete
  4. Mzee wa miundombinu......akizidi kumnanga Manara atajikuta anaanikwa maovu yake na mwendazake maana anajua yote aliyokuwa anayafanya yeye na Kaburu

    ReplyDelete
  5. Uyu ni mmoja ya viongoz walioinjinia usajili wa Morrison kwa kuwaingiza chaka wenzake sasa ngoja tuone kitachofata

    ReplyDelete
  6. Kwa suala la Morrison mtasubiri sana

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mkwanja wetu wa nguvu tuautaka! Mtaona faida ya ukanjanja wake

      Delete
  7. Sawa uncle kasepa ila kuwahi waungwana basi mpeni walao kiinua mgongo maana kaitumikia simba kwa nguvu zote

    ReplyDelete
  8. Msimu uhao Wataishia kwenye makundi kama walivyotolewa na UD Songo

    ReplyDelete
  9. Wakishatplewa mapema waseme next level pia, wasijikaushe, hapo ndio tambo za Manara Vs Wadosi mtaziona

    ReplyDelete
  10. Hata huko baada ya kugaragazwa mapema watayafanya yale yale ya ubabe kusema refa kawaonea na kupiga kupiga ngumi kama vile walipompiga Bocco wanapoona wameelemewa halafu kufunguwa kesi fifa kwakujiona wao majabari hawaogopi chochote. Ama kwa matusi Mungu awazidishie

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic