July 6, 2021


 HAJI Omari Mpili, maarufu kama Mzee Mpili amesema kuwa hawezi kushindana na Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara kwa kuwa ni mtoto mdogo na lazima ataifunga tena Simba watakapokutana kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho.

Mzee Mpili amebainisha kuwa ushindi wao wa Julai 3 yeye alikuwa ni mchezaji namba moja kwa kuwa ana watu hivyo hana mashaka na mchezo wao kuelekea Julai 25 na amesisitiza kwamba lazima alipwe mkwanja ambao aliahidiwa na Manara ambao ni milioni moja.

"Mimi ninasema kwamba mchezo wetu ule pale taifa nilikuwa mchezaji namba moja na kuelekea kwenye mchezo wetu Kigoma nina amini kwamba nitaucheza na tutashinda.

"Siwezi kushindana na Manara, yeye ni mtoto mdogo haniwezi na mimi nina watu wakubwa kila mahali, sasa ninasema hivi kwa kuwa aliniahidi atanipa milioni moja ninaitaka.

"Yeye mwenyewe Manara alisema kuwa ohh Mzee Mpili ukitufunga sisi nitakupa milioni moja, basi sikumuomba mwenyewe amesema naitaka milioni moja yangu na ninasema kwamba Kigoma tunashinda tena," amesema.

Katika mchezo wa Julai 3, Simba ilishuhudia dk 90 ubao wa Uwanja wa Mkapa ukisoma Simba 0-1 Yanga na bao pekee la ushindi lilifungwa na Zawad Mauya dk 12.

9 COMMENTS:

  1. Dahh!!!! Jamani imetosha na huyu mzee Mpili......khaaaaa!

    ReplyDelete
  2. Bora yeye mwenyewe anekiri kuwa alikuwa mchezaji namba moja, hata like shuti alipiga yeye kupitia uchawi wake, ndio alimfumbaza refa asione penati zile, ndio alikuwa golini anapeperusha na kudaka mashuti ya wachezaji wa simba. Kweli uchawi duniani upo. Kimpira utopolo hana uwezo wa kuifunga simba.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kama u naamini katika hilo ushafilisika kiakili

      Delete
    2. Yaani huyu jamaa amekomalia suala la uchawi hadi kichwa kinamuuma...Nina wasiwasi hata mafanikio ya majirani zake mtaani anayaonea wivu na kuwaendea kwa waganga kutokana na jinsi anavyoonesha kuuabudu uchawi.Kama anadhani uchawi ndio suluhisho basi awasaidie Simba kupanga tunguri uwanjani zicheze.Ukishakuwa na imani tele kwenye nguvu za giza usitegemee maendeleo yoyote

      Delete
    3. Watu wanasema eti mashuti waliopiga simba, kwani walipiga mangapi?

      Shot on target
      Simba 2 na Yanga 4
      (PAMOJA NA GOLI)

      Shot off target
      Simba 4 na Yanga 6

      Coner
      Simba 6 na Yanga 5

      Offside
      Simba 0 na Yanga 1

      Yelow card
      Simba 2 Ynga 3

      Foul
      Simba 21 na Yanga 12

      KWENYE HILI ONYANGO NA WAWA WANAJUA, WE BONGO LALA ANGALIA TAKWIMU YALIYOLENGA LANGO 2 TU, USISAHAU ZANZIBAR
      SHOT ON TARGET
      SIMBA 0 YANGA 13
      KAJIFUNZE AU KAANGALIE MARUDIO

      Delete
    4. Usione aibu kuweka ball possession

      Delete
    5. Ball possession sio kigezo pekee cha timu kuwa bora katika mchezo husika,inategemea pia na mbinu za timu pinzani katika game approach

      Delete
  3. Mechi kati ya Kaizer Chiefs na Simba mpaka dk 70 ball posession ilikuwa simba 69 kaizer chief 31 ila magoli yalikuwa simba 0 kaizer 3

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic