October 11, 2021


 KINARA wa chati ya wafungaji bora kwenye Ligi Kuu Bara mpaka sasa, Reliants Lusajo amefunguka kuwa malengo yake makubwa ni kuhakikisha anafunga mabao mengi zaidi msimu huu ili kutimiza ndoto yake ya kutwaa kiatu cha ufungaji bora ambacho kinatetewa na nahodha wa Simba John Bocco.

Lusajo katika michezo miwili iliyopita ya Namungo amefanikiwa kufunga mabao mawili, akifunga bao moja kwenye mchezo dhidi ya Kagera Sugar na mchezo dhidi ya Geita Gold. 

Mshambuliaji huyo msimu wa 2019/20, akiwa na kikosi cha Namungo alifanikiwa kuibuka mfungaji bora namba nne naada ya kufunga mabao 12.


Akizungumza na Championi Jumatatu, Lusajo alisema: “Kama kikosi tumekuwa na mwanzo mzuri wa msimu huu ambapo mpaka sasa hatujapoteza mchezo wowote katika michezo yetu miwili ya kwanza, lakini nafurahi pia kuanza vizuri kwa kufunga mabao mawili katika michezo hiyo.


“Malengo ya kila mshambuliaji ni kuhakikisha anafunga mabao, hivyo natumaini nitaendelea kuwa katika kiwango bora kama ilivyo sasa, na kufunga mabao mengi ili kutimiza malengo yangu ya kushinda tuzo ya mfungaji bora.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic