July 27, 2013

Matumaini ya Watanzania kwa Taifa Stars huenda ingeweza kubadili matokeo mjini Kampala na kusema mbele kucheza Kombe la Chan mwakani nchini Afrika Kusini, yameishia hewani.
Stars imelalala kwa mabao 3-1 dhidi ya wenyeji wake The Cranes mjini Kampala na kufanya iwe imepoteza kwa jumla ya mabao 4-1.
Stars ambayo ilipoteza mechi ya kwanza kwa bao 1-0 jijini Dar, leo ilikwenda mapumziko ikiwa na inaongoza kwa bao moja lililofungwa na Amri Kiemba.
Lakini kipindi cha pili Waganda walionekana kubadilika na mapema tu wakapata bao la kwanza na bao la pili lililofungwa kwa mkwaju wa penalti.
Kosa la kuzubaa na mpira wakati Stars inashambulia kuliifanya Uganda ifanye shambulizi la kushtukiza na kufunga kwa ulaini bao la tatu.
Baada ya hapo, wenyeji walionekana kupoteza muda huku wachezaji wa Stars wakimlalamikia mwamuzi kutokana na kuonyesha wazi alitaka wenyeji washinde.
Mara ya mwisho The Cranes kupoteza mechi katika Uwanja wa Namboole ilikuwa ni mwaka 2004 walipofungwa na Afrika Kusini na baada ya hapo wamekuwa wakishinda au kutoka sare.
Hata hivyo, Stars pia ilionekana kukosa mipango kila ilipofika mbele kama ilivyokuwa katika mechi ya kwanza jijini Dar.
Wachezaji wa Stars waliendelea kucheza kama wale waliokata tamaa kabisa na mara nyingi walipokonywa mipira karibu kila mara.

Baada ya mwamuzi kupuliza kipenga cha mwisho, Kocha Mkuu, Sredojevic Milutin 'Micho' aliyewahi kuinoa Yanga alionekana kuchanganyikiwa kwa furaha na kukimbia kama mwendawazimu.
Mara ya mwisho Stars ilicheza michuano ya Chan mwaka 2009 nchini Ivory Coast na ikatolewa katika hatua ya robo fainali baada ya kutoka sare ya bao 1-1 na Zambia mjini Bouake.

1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic