April 21, 2019


Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema timu yake bado ina nafasi ya kutwaa ubingwa msimu huu lakini inabidi wapate ushindi katika michezo sita iliyobaki.

Zahera amesema wanahitaji kushinda michezo yote sita iliyobaki ikiwa ni dhidi ya Azam FC, Ruvu Shooting, Biashara United, Mbeya City, Tanzania Prisons na Azam FC

"Ligi bado iko wazi hakuna timu ambayo imejihakikishia ubingwa.

"Kwa upande wetu hatupaswi kufanya makosa zaidi kwenye michezo iliyobaki ili kuwa na nafasi" amesema Zahera.

Ukiondoa mchezo dhidi ya Biashara United ambao utapigwa mkoani Mara, habari njema ni kuwa michezo mingine mitano itapigwa uwanja wa Taifa

Yanga itarudi Dar kumalizia michezo yake ya nyumbani iliyobaki baada ya michuano ya AFCON ya vijana kumalizika Aprili 28 2019

Aprili 29 Yanga itaanza kampeni ya kusaka ushindi katika michezo hiyo kwa kuikabili Azam Fc katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Taifa.

Yanga ina michezo miwili dhidi ya Azam Fc na pengine mchezo huo wa April 29 utabainisha hatma ya vinara hao wa ligi katika mbio za ubingwa

Baada ya mapumziko ya Pasaka, kikosi cha Yanga kitaendelea na maandalizi kuelekea mchezo dhidi ya Azam FC ambao utapigwa Jumatatu ijayo

2 COMMENTS:

  1. mm binafsi ni shabiki na kipenzi cha Dar Young Africans but suala la ubingwa ni less than 10% kwa timu yetu makosa n kila mechi kuruhusu goal

    ReplyDelete
  2. Wewe Kocha Zahera wekeza muda mwingi kwenye mazoezi na kukisuka kikosi chako acha kutumia muda mwingi kujibizana na akina Manara, TFF na Bodi ya Ligi, acha lawamalawama....timu yako bado hairidhishi ingawa inashinda kwa taabu wakati mwingine hutoa sare na hata kufungwa....Naomba mfikishieni ujumbe huu tafadhalini

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic