July 27, 2013

Kiungo nyota wa Real Madrid, Xabi Alonso amerejea mazoezini kwa mara nyingine ikiwa ni zaidi ya mwezi mzima kuwa nje ya uwanja.
Alonso alikuwa nje ya uwanja kutokana na kufanyiwa upasuaji na sasa ni kati ya wachezaji walio katika mazoezi ya timu hiyo inayojiandaa kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya PSG, leo.
Madrid wameonekana kuwa na faraja kubwa baada ya kiungo huyo aliyezaliwa katika eneo la Tolosa kurejea tena mazoezini.

Kwa upande mwingine, taarifa kutoka katika uongozi wa Real Madrid zimeeleza kuwa kiungo Mbrazil, Kaka amekuwa akiendelea vizuri zaidi na kuwapa matumaini kuwa atarejea katika kiwango chake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic