March 23, 2014


CHALE


SIKU moja baada ya kukumbana na kipigo cha mabao 3-0 kutoka kwa Yanga, Kocha Mkuu wa Rhino, Jumanne Chale amesema wako baadhi ya wadau we mkoa we Tabora wanachangia timu hiyo kutofanya vizuri.

Chale amesema amekuwa akishangazwa na kuona baadhi ya mashabiki au wadau wa soka katika mkoa huo wakifanya kila juhudi kuzisaidia timu za wageni.
“Wanaona Yanga, Simba au timu nyingine ndiyo wanapaswa kuzisaidia. Lakini wanasahau wao wako hapa Tabora.
“Hata kuziona timu nyingine ni kwa kuwa Rhino iko ligi kuu. Ikiteremka wataziona wapi Yanga na Simba, kweli inanishangaza sana,” alisema akionyesha kutokukubaliana na suala hilo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic